JIPE TUMAINI JIPYA MAANA KESHO IPO

Imeandikwa na Joche toka JocheApp

Habari Ndugu mfuatiliaji na msomaji wa makala zetu za kuelimisha na kuhamasisha watu mbalimbali kupitia Application yako ya JOCHEAPP

Leo natamani kuongea na wapambanaji katika changamoto za kila siku katika ulimwengu huu uendao kasi na mambo yake

Awali ya yote niwapongeze wanafunzi wote wale walio katika mfumo wa kikanuni yaani rasmi wa kukaa darasani na hata wale ambao hawakai darasani lakini wanajifunza...

Nisiwasahau kuwasalimia na kuwatia moyo wale ambao hawajapata cha kufanya maana wanaona hawana kazi wala hawasomi.... nina neno moja Kwenu FANYA KAZI YOYOTE malipo/faida ni kama ZAWADI usikubali kukaa bila kuwa na lakufanya.

Siku ya Leo nina jambo moja natamani kukuambia nalo ni:-

USIPOTEZE TUMAINI KWA JAMBO/MAMBO ULIYOYAPATA LEO,  HUWEZI IJUA SIKU YA KESHO INAVITU GANI

Hapa kwenye tumaini ni eneo la msingi sana kama kijana kuwa nalo... 

Haijalishi uliuza Ubuyu ukaharibikia dukani haukuisha na leo umeenda umekuta umeshatia ukungu, usivunjike moyo inua moyo wako jipe TUMAINI kesho ipo usikate tamaa

Haijalishi ulifuga mifugo ikafa au walivunja wakaiba na kuondoka nayo... usikate Tamaa Jipe Tumaini Kesho inakuja inuka na anza hapo ulipokwamia utavuka tuu

Haijalishi ulilima na mvua zikagoma... piga hesabu zako upya anza tena usipoteze Tumaini kesho inakuja

Haijalishi shule inakwama na unapata matokeo ambayo sio mazuri suluhisho sio kuacha ila kaza mwendo ungeza bidii utavuka

Mwanafalsafa mmoja alisema... HUWEZI KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOKUKABILI KWA KUTUMIA AKILI/NJIA/MPANGO ULE ULE ULIOLETA HIYO CHANGAMOTO

Maana yake ni nini?

Ili uweze kuvuka changamoto inayokufanya usisogee mbele ni lazima utafute maarifa ya zaidi kuliko changamoto inayokusumbua na kukufanya usipige hatua.

Soma Vitabu vyenye mlengo wa eneo ambalo unafanya litakusaidia kukuimarisha na kukuinua zaidi.

Soma VITABU SAHIHI ni  chakula cha Nafsi/Roho ili kuiimarisha roho yako isimame upya kwa ujasiri mpya na Roho wa Mungu akiwa Pamoja nawe...

Epuka Marafiki wasio na faida katika maisha yako.

Pata muda wa kujikagua kwa kila hatua unayopiga katika Maisha yako.

 NIKITAKIE WAKATI MWENA NDUGU YANGU.

*NEVER LOSE HOPE, TOMMOROW IS COMING*

TUKUTANE TENA WAKATI MWINGINE MUNGU AKITUPA UZIMA.

_______________________________________
Mwandishi: Joseph Geotham Mrema
Mawasiliano: +255 712851687
Barua Pepe: josephgeotham4@gmail.com
Application: JOCHEAPP

_______________________________________

No comments

Featured post

MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI

 MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI 1.Kuhudumiwa na Mtu anaye SMILES. Humfanya mteja ajihisi yuko huru zaidi kuuliza na kuamini unaweza k...