UJUMBE KWA KIONGOZI/ KIONGOZI MTARAJIWA

Uongozi ni jukumu ambalo mtu hupewa na watu ili kusimamia jambo fulani kwa niaba ya watu fulani.

Kiongozi kwa kushirikiana na watu wake anaweza kufanikisha mahitaji ya watu wake.

Kiongozi akilewa na madaraka hufikia hatua ya kufanya maamuzi pasipo kushirikisha watu wake na hilo hupelekea kutofanikisha mahitaji ya watu wake bali kufanikisha mahitaji yake binafsi.

Kiongozi mwenye nidhamu na watu wake anauwezo wa kujiamini na kukiri kosa pindi akoseapo na kuamua kutafuta namna ya kuweka mambo sawa ili amani idumu kwa watu wake.


Mtu hawezi itwa kiongozi kama hana wakumuongoza, kwa maana hiyo watu ndio humfanya kiongozi ajulikane kuwa kiongozi.

Jitahidi kuweka vema watu wako ukiwa kama kiongozi epuka kuongoza kimabavu, jifunze kujishusha ili watu wako na Muumba wako wakukweze kwa wakati .

Asante
JERRY JERRY

Visit Us: JOCHE APP

No comments

Featured post

MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI

 MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI 1.Kuhudumiwa na Mtu anaye SMILES. Humfanya mteja ajihisi yuko huru zaidi kuuliza na kuamini unaweza k...