KUELEKEA PALE

Maisha  yanafananishwa  na safari  kama  zilivyokuwa  safari nyingine.Kila mmoja  wetu anapambana  hapa na pale  ili aweze  kufikia  katika  hatma  yake.Katika  safari yoyote  ile ni lazima  kuwe na dhoruba na adha za aina mbalimbali.  Kwamfano, katika barabara unaweza 
kukutana  na milima, mabonde  na makorongo. Katika  maji unaweza  kukutana  na mchafuko hali kadhalika  ukitumia  usafiri  wa anga  unaweza   kukutana  na hali mbaya ya hewa.Lakini pamoja  na haya yote huwa tunafanikiwa  kufika  katika  yale maeneo  tunayoelekea.Vivyo  hivyo katika  maisha kuna muda  tunapitia  changamoto  kali na ngumu  kiasi  cha kukata  tamaa...kuna changamoto  za kiuchumi,kisiasa, kiroho,kijamii  na nyingine  nyingi. Katika hizi zote  yamkini kuna watu tuliowategemea  sana  na wakageuka  kuwa  miiba. Kuna usemi  mmoja wa lugha  ya kiingereza  unaosema,"the world  is a  classroom  and every  person  you meet  is a  teacher "

Unapokutana  na kuona  watu hawapo  pamoja  na  ww  usiwalaumu wala kuwachukia. Unapaswa  kutambua  na kuamini  kwamba  ipo hivyo  ilivyo  kwa ajili  ya  kukujenga  na kukufanya  uwe bora zaidi. Katika  kila gumu unalolipitia  linakutengeneza  na kukufanya  uwe  bora  zaidi,kwani hauwezi  kuimarika  bila kubomoka, kutingishwa  na mengine  mengi  yafananayo  na haya.Swali la kujiuliza, Je,nifanye  nini wakati  ninapokuwa  napitia  magumu  ili nisiiharibu  safari  yangu?Kuna  mengi sana ya kufanya  juu ya  hili lakini  kwa ujumla unapaswa  kujua  wewe  ni nani? Unatoka  wapi? Unataka  nini?Unaelekea  wapi?Pamoja  na kuwa na  tumaini, imani na uvumilivu. Ukijua  unachokitaka  utapambana  mpaka  uone mwisho  wako.Pia unapaswa  kujitamkia  mema na ushindi  kutoka  ndani yako kwani tuna nguvu ya uumbaji. ...jipe  moyo jiambie  ni naweza, ntapambana  na nitafika  hata iweje.
Kuna siku utasimama  na kufurahi  na kusema ni kwa sababu  sikukata  tamaa  na kuishia njiani .
Inawezekana #Jiamini 
# pigania ndoto zako
# una nguvu. 
#ririwords

JocheApp
________________________________________________


JocheApp

No comments

Featured post

MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI

 MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI 1.Kuhudumiwa na Mtu anaye SMILES. Humfanya mteja ajihisi yuko huru zaidi kuuliza na kuamini unaweza k...