THAMANI NDANI YA MTU

Habari za saa ndugu  msomaji. .. ni matumaini  yangu unaendelea  vizuri  ktk mapambano  ili uweze  kufikia  ndoto  na malengo  yako.

Huko Italy kulikuwa  kuna jiwe moja ambalo ndani ya hilo jiwe ilitakiwa  kuchongwa  sanamu  ya Daudi. 

Kuna watu wawili ambao  ni Agustino  na Antonio  walipewa  kazi  ya kuchonga  sanamu  hiyo..lakini  walishindwa  wakasema  jiwe hilo haliwezi  kutoa  sanamu  nzuri.

Baada ya miaka  25 baadae  kazi hii alipewa  mtu aliyeitwa  Michangelo. ..baada  ya  miaka  mitatu  alikuwa  ameshamaliza  kuchonga  na alipata  sanamu  nzuri tu  na ilikuwa ni mwaka  1504.Sanamu hiyo ni kivutio  cha watalii  wengi mpaka leo hii .Mamilioni  ya watalii hufika  na kuitazama  sanamu hii.

Siku moja papa  akamuuliza  umewezaje  kupata  sanamu  ndani  ya  jiwe hili? 
Naye akajibu, akasema  nilimuona  Daudi  tayari  ndani ya  jiwe  hili hivyo nilichokifanya  ni kutoa  kile  ambacho  si Daudi  ili Daudi  abakie  na aonekane  vizuri.
Kutokana  na habari  hii fupi kuna mengi sana  ya  kujifunza  lakini  kwa leo tuangalie  kwa ufupi mawili  matatu.

Yamkini  kwenye maisha  kuna watu  ambao wanakudharau  na wanakuona  si kitu...hao ni kina Antonio  na Agusto. kamwe  usiwaruhusu  wakufanye  ujione  wewe  si kitu,huna thamani  na hauwezi  kwani ndani  yetu  kila  mtu  amewekewa  kitu cha thamani  sana na Mungu kwa ajili  ya  kutimiza  kusudi  lake  hapa duniani.
Lakini pia kuna watu ambao ni Michangelo  ktk Maisha  yako. ..kuna watu  wanaona  vitu vikubwa  ndani yako,kuna  watu ambao  wanapambana  sana kuwa karibu  yako ili waondoe  vile ambavyo  sio wewe  ili ubakie  wewe.Yamkini  watu hawa wameletwa  na Mungu  kwenye  maisha  yako, Je,ni mara ngapi  umewafukuza, umewatusi, umewadharau  na kuwaumiza  akina  Michangelo? Pengine  ni katika  huduma,mahusiano  elimu  na mambo mengine?

Na ni mara ngapi umechukua  jukumu  la kuwa Michangelo  wako mwenyewe?ukaangalia  yale mambo  yote  mabaya  yanayokufanya  usiwe halisi?
Chukua  hatua sasa.


Tafakari 
Jiulize 
Sikiliza  hizo sauti.
#ririwords
#theroadtothere

JocheApp
________________________________________________

JocheApp

No comments

Featured post

MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI

 MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI 1.Kuhudumiwa na Mtu anaye SMILES. Humfanya mteja ajihisi yuko huru zaidi kuuliza na kuamini unaweza k...