SEASON 2
SEHEMU YA 18
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Nilitegemea baada ya kipigo cha siku ile basi asingerejea tena kwa Peniela lakini bado hajakoma na amerejea tena.Huyu jamaa ana mke wake kwa nini anaingilia mali za watu? Peniela ni mpenzi wangu mimi na sintokubali Elibariki anipindue na siwezi kukubali aendelee kukaa pale kwa Penny.Siwezi kukubali aendelee kukaa na mwanamke ambaye nimemuhangaikia mpaka nikamuweka huru.Ninampenda Peniela na kwa ajili yake niko tayari kwa lolote.Nikizubaa ninaweza kunyang’anywa mtu wangu hivi hivi nikiona.Lazima nipambane na Elibariki.lazima nimtoe kwa Peniela na asikanyage tena pale.Najua atakuwa amemdanganya Peniela kwamba yeye ndiye aliyemuachia huru.Mimi ndiye niliyefanikisha hadi peniela akaachiwa huru.Bila mimi kusimama imara na kutoa ushahidi wenye nguvu asingepata nguvu ya kumuachia huru peniela.Nilipambana kufa na kupona kwa sababu ninampenda Peniela.Vita hii na Elibariki haitakwisha na lazima nimuonyeshe kwamba sisi ndio watoto wa mji huu” Akawaza Jason
ENDELEA……………..
“ Sikuwahi kuota kama Peniela anaweza akawa ni msichana mrembo namna hii.Dah ! ni kama ninamuona malaika” akawaza jaji Elbariki akiwa kitandani akimshuhudia Peniela akijiandaa kwa ajili ya kutoka.
“ Moyo unaniuma sana kutokujua mahala anakokwenda Peniela. Anakwenda kuonana na nani? Ninasikia wivu mkubwa labda kuna mwanaume anakwenda kuonana naye.Siwezi kuvumilia atakaporudi leo lazima nimuulize ili nifahamu mahala anakokwenda” akawaza jaji Elibariki akimuangalia Peniela akimalizia kujipodoa.Alikuwa amevaa gauni refu jekundu lililompendeza sana.
“ Elibariki I have to go now.Nitarejea baadae kidogo kuna mtu nahitaji kuonana naye usiku huu” akasema Peniela huku akitabasamu
“ Ni mchumba wako? Akauliza jaji Elibariki
“ Hapana si mchumba wangu.Nilikwambia kwamba sina mchumba.Ni mtu ambaye nina maongezi naye ya kibiashara” akasema Peniela na kumsogelea jaji Elibarki akambusu
“ Don’t open the door to anybody” akasema Peniela
“ Usijali Peniela sintafanya hivyo na hakuna yeyote anayeweza kujua kama niko hapa” akasema Elbariki na Peniela akachukua funguo za gari lake akatoka na kulitoa gari lake gereji akafungua geti na kutoa gari nje kisha akafunga geti kwa kufuli kubwa ili yeyote atakayekuja ajue kwamba hakuna mtu mle ndani.
“ Kuna kitu nimekigundua kwa Elibariki.Hakufurahishwa na mimi kuondoka usiku huu.Macho yake yanaonyesha alikuwa anaona wivu mkubwa.He loves me.Kwa hilo sina shaka nalo hata kidogo.Lakini sitaki afahamu kwamba nina mahusiano na baba mkwe wake.Akigundua jambo hili nitampoteza .Sitaki hilo litokee na nitafanya kila linalowezekana ili Elibariki asiweze kugundua chochote kuhusiana na mahusiano yangu na rais.Ninamuhitaji sana na hatabanduka katika mikono yangu” akawaza Peniela akiwa katika mwendo mkali kuelekea katika nyumba aliyopewa na Dr Joshua
Aliwasili katika jumba lile lililokuwa kandoni mwa bahari.Katika geti la kuingilia kulikuwa na vijana wawili waliokuwa wamevalia suti nzuri nyeusi,Penny akawatambua vijana wale ni walinzi wa rais akasalimiana nao wakamfungulia geti akaingia ndani.Akaegesha gari na kufungua mlango akawasha taa
“ The house is too quiety and big for me” akawaza Peniela na kuelekea moja kwa moja katika chumba cha kulala na kukaa kitandani akachukua simu yake na kumpigia Dr Joshua ili kumtaarifu kwamba tayari amekwisha fika lakini simu ya Dr Joshua ikaita bila kupokelewa.
“ Mbona hapokei simu? Labda atakuwa kwenye kikao.” Akawaza penny na kisha akampigia simu Kareem mlinzi wa Dr Joshua na kumuomba amtaarifu Dr Joshua kwamba tayari amekwisha wasili pale nyumbani.
Saa tatu kasoro dakika kumi mlango mkubwa wa sebuleni ukafunguliwa wakaingia walinzi wanne wa Dr Joshua halafu baada ya muda akaingia Dr Joshua mwenyewe
“ thank you guys” Dr Joshua akawaambia wale walinzi wake halafu wawili wakatoka na kusimama nje ya mlango , wengine wawili wakaongozana naye hadi katika chumba cha kulala alimo Peniela.Akagonga mlango na ukafunguliwa na Peniela.Dr Joshua akaingia ndani wale walinzi wake wakasogea mbali kidogo na pale chumbani
Peniela akamrukia Dr Joshua na kumkumbatia kwa furaha kubwa na kuanza kumporomoshea mabusu mazito.Dr Joshua akapagawa.
“ Dr Joshua I missed you so much my love” akasema Peniela
“ I missed you too peniela.I missd you so badly” akasema Dr Joshua huku akihema mfululizo .Peniela akamvua koti halafu akamfugua tai na kumvuta kitandani
“ Dr Joshua nimekuita hapa kwa kazi moja tu.To make me happy” akasema Peniela na kulivua gauni lake akabaki mtupu.Dr Joshau akazidi kupagawa .Damu ilimchemka.Peniela alisisimua kumuona akiwa mtupu
Dr Joshua alishindwa kuendelea kusubiri zaidi kwani hata yeye alikuwa na hamu sana na Peniela,akamvuta na shughuli ikaanza.Baada ya dakika kumi mzunguko wa kwanza ukamalizika.Dr Joshua alikuwa akihema kwa kasi.Mwendo aliopelekwa na Penny haukuwa mdogo
“ Nina bahati sana ya kukupata Peniela.Unajua kunifurahisha.Unajua kunipa raha.Kwa ajili yako niko tayari kukupa kitu chochote kile.Umeifanya akili yangu ikuwaze kila sekunde.”akasema Dr Joshua kijasho kikimtiririka.Peniela aliyekuwa pembeni yake akatabasamu na kumbusu kisha akasema
“ Dr Joshua kuna jambo nataka nikuombe”
“ Omba chochote peniela.Kitu chochote ukitakacho nitakupatia”
“ Ahsante sana Dr Joshua na ndiyo maana nakupenda,unajua kujali.laiti kama wanaume wote wangekuwa kama wewe wanawake tungesikia fahari kubwa sana.” akasema Peniela na uso wa Dr Joshua ukajenga tabasamu.
“ Mimi ni namba moja hapa nchini na kila kitu kiko chini yangu.Unataka nikupatie kitu gani? Chochote ukitakacho nitakupatia” akajigamba Dr Joshua
“ Dr Joshua,nina mjomba wangu ambaye ni mgonjwa sana na anahitaji kufanyiwa upasuaji wa kichwa.” Akasema Peniela na kumstua Dr Joshua
“ kwa nini siku zote hizi hujaniambia kama una mjomba wako anaumwa? Ningekwishamsafirisha kwenda nje ya nchi kwa matibabu.”
“ Ahsante sana Dr Joshua lakini hakuna haja ya kumpeleka nje ya nchi.Yeye ana marafiki zake ambao ni madaktari wanatoka je ya nchi watakuja kumfanyia upasuaji huo kwa hiyo wanachohitaji wao ni kupata hospotali yenye vifaa vya kuwawezesha kumfanyia upasuaji huo.Kwa kuwa wewe una nguvu na sauti ninaomba unisaidie kuweza kupata hospitali hiyo ili mjomba wangu aweze kufanyiwa upasuaji huo.” Akasema Peniela.Dr Joshau akamsogeza kwake akambusu na kusema
“ Siku nyingine kama una tatizo lolote hata liwe kubwa kiasi gani usisite kuniambia.Mimi niko kwa ajili yako na nitakufanyia chochote kile unachokitaka.Usijali kuhusu ombi lako.Kuna hospitali moja nzuri sana imefunguliwa hivi majuzi hospitali hii ndiyo hutumika kututibu sisi viongozi wa serikali.Ni hospitali yenye kila kifaa na wataalamu.Huna sababu ya kuwa na wasi wasi.Mjomba wako atatibiwa pale na atapona tu”
“ Nashukuru sana Dr Joshua lakini kuna jambo moja nataka nikuombe kuhusiana na suala hili” akasema peniela
“ peniela wewe ni first lady omba chochote kile.Nchi hii ni ya kwetu” akasema Dr Joshua.Peniela akatasamu na kusema
“ Ninaomba jambo hili liwe la siri kubwa na hata upasuaji huo ufanyike kwa siri na muda wote ambao mjomba wangu atakuwa akitibiwa pale hospitali basi kuwe na usiri mkubwa.Unaweza ukanisaidia na hili pia? Akauliza Peniela.Dr Joshua akafikiri kidogo na kusema
“ Huyo mjomba wako ni nani? Kwa nini atibiwe kwa siri? Akauliza .
“ Ni mtu ambaye hapendi famiilia yake ifahamu kuhusiana na upasuaji huo kwa hiyo anataka aufanye kwa siri bila ya mtu yeyote kufahamu.”
“ usijali Peniela.Kwa ajili yako kila kitu kinawezekana.Nitawasiliana na daktari mkuu wa pale na nitakuunganisha naye ili maandalizi yaweze kufanyika.Utapata kila unachokihitaji”
“ Asante sana Joshua” akasema Peniela na kuanza kuzichezea nyeti za Dr Joshua kwa ufundi mkubwa hukuDr Joshua akitoa migumo kwa raha aliyokuwa akiipata.Alishindwa kuvumilia wakaingia tena katika mzunguko mwingine
*******
Anitha hakuwa akijisikia kuinuka pale sofani alipokaa.Alihisi mwli wake wote hauna nguvu hata kidogo.Bado alikuwa na mawazo mengi sana kuhusiana na kifo cha Noah.Macho yake bado yaliendelea kutoa machozi kila alipomkumbuka Noah.Taratibu akainuka na kuelekea chumbani kwa Noah ambako Mathew alikuwa akipakia vitu vya Noah katika sanduku kwa ajili ya kuwakabidhi ndugu zake hapo kesho.
“ N vigumu kuamini kama kweli Noah hatuko naye tena”akasema Mathew
“ Inauma sana Mathew.Inaniuma sana” akasema Anitha.Mathew akaacha ile kazi aliyokuwa akifanya akamshika Anitha mkono na kumketisha kitandani.
“ Anitha kama nilivyokwambia awali kwamba lazima tukubaliane na ukweli kwamba Noah amekwenda na hatutamuona tena hadi siku hiyo ya mwisho.Kitu kikubwa ambacho tunaweza kukifanya kwa sasa katika kumuenzi ni kuwatafuta wale wote waliomuua.lazima tuendeleze mapambano na tusimame imara kuhakikisha kwamba kazi tuliyoianza tunaimaliza .Pamoja na maumivu tuliyonayo lakini lazima tuendelee na kazi yetu na kazi kubwa kwa sasa ni kuwabaini wale wote waliofanya kitendo hiki na tunaweza tu kuwapata kwa kuhakikisha kwamba Elibariki anaendelea kuwa salama.Ni yeye ndiye anayeweza kutupa picha kamili nini hasa kilitokea siku ile na nina hakika anaweza kuwa anawafahamu wauaji.”akasema Mathew.Anitha akafuta machozi na kumtazama Mathew
“ Kwa hiyo tutafanya nini Mathew kumlinda Elibariki?Nina wasi wasi sana na maisha yake.”Akasema Anitha
“ Kuna kitu ninakifikiria.Tunahitaji kuonana na Elibariki na kumshawishi awe kuja hapa kwetu ambako ni salama zaidi kuliko kule kwa Peniela.Kwa kuwa wewe hujisikii vizuri na umechoka mimi ngoja nikaonane naye usiku huu halafu nitakwambia ni kitu gani tumeongea.Nitakaporudi nitakuwa na jibu la nini kinaendelea “ akasemaMathew
“ Hapana Mathew siwezi kubaki hapa peke yangu.Ninaogopa sana.Hata kama sina nguvu lakini nitaongozana nawe.” Akasema Anitha
“ Are you sure? Akauliza Mathew
“ yes I’m sure” akajibu Anitha.
Dakika kumi baadae wakaingia garini na kuondoka kuelekea nyumbani kwa Peniela
“ Mke wa Elibariki anafahamu kama mume wake yuko kwa Peniela? Akauliza Anitha wakiwa garini
“ Sina hakika kama anafahamu .Elibariki hawezi kuwa mjinga na kumueleza mke wake kwamba amejificha kwa mwanamke mwingine.” Akajibu Mathew
“ lakini wanaume ! kwa nini anamfanyia hivi mke wake?
“ Anitha wewe hauko katika ndoa na huyafahamu mambo yaliyomo ndani ya ndoa.Nina hakika siku na wewe ukiingia katika ndoa yanaweza yakakukuta kama yanayomkuta mke wa Elibariki” akasema Mathew na kumfanya Anitha acheke.Ilikuwa ni mara ya kwanza Anitha anacheke toka ulipotokea msiba wa Noah.
“ Hii ndiyo sabau ambayo inanifanya nisitake kabisa kuolewa.Sitaki matatizo kama hayo.Napenda niishi mwenyewe .Nahisi amani na furaha .Wanaume siku hizi wamekuwa wadanganyifu sana”
“ Si wanaume tu hata wanawake nanyi siku hizi mmekuwa na udanganyifu mkubwa.Hakuna mkweli zama hizi.Wote tundanganyana tu” akasema Mathew
“ Lakini usikate tamaa Mathew siku moja unaweza ukapata mwanamke ambaye atakufaa.Wanawake wazuri bado wapo”
“ Jambo hilo nimekwisha litoa kabisa katika akili yangu.Nilimpenda mwanamke mmoja tu na alipouawa aliondoka na mapenzi yote na sina tena mapenzi kwa mwanamke mwingine yeyote” akasema Mathew
“ Hata mimi hunipendi? Akauliza Anitha na kumfanya Mathew acheke kicheko kikubwa
“ Usinichekesha Anitha.Niache kukupenda wewe? Wewe ni kila kitu kwangu kwa sasa.Kupenda nilikokuwa nakuongelea ni kutafuta mwanamke wa kuishi naye.”
“ Ikitokea ukanipenda ninafaa kuwa mke? Akauliza Anitha na kumfanya Mathew azidi kucheka.
“ Anitha leo umenifurahisha sana.Mimi na wewe katu hatuwezi kufika huko. “
“ kwa nini hatuwezi kufika huko? Kwani sisi tumekosa nini? Akauliza Anitha
“ Sisi tuko tofauti sana.” Akasema Mathew
“ Unajua mathew kuna kitu nimejifunza kutokana kifo cha Noah.”
“ Kitu gani? akauliza Mathew
“ Noah amekufa bado kijana mdogo sana na hakuweza kutimiza malengo yake mengi.Maisha haya ni mafupi na hakuna anayefahamu nini kitatokea kesho.Noah amekufa hana mke wala mtoto.Hana kumbu kumbu yoyote aliyoiacha hapa duniani.Kazi hizi zinatufanya tunajisahau kabisa kwamba tunahitaji na sisi furaha maishani.We need to be happy.Tusijisahau kabisa na tukafa kifo kama cha Noah.Nimetafakari sana kuhusu jambo hili na kuna jambo nimelifikiria ”akasema Anitha
“ Jambo gani Anitha ? akauliza Mathew wakati akikata kona kuingia katika mtaa anaoishi peniela na mara ghafla akafunga breki ..
“ Kuna nini? Akaulizia Anitha
“ Ouh my God !..akasema Mathew .Anitha naye akaelekeza macho yake mbele.Katika geti la nyumba ya Peniela kulikuwa na kundi la askari polisi waliojihami kwa silaha.
“ Pale ni nyumbani kwa Peniela “ akasema Mathew
“ Askari wale wanatafuta nini pale kwa peniela? Akauliza Anitha
“ Ninahisi kuna jambo limetokea au tayari wamekwisha fahamu kwamba Elibariki yuko mle ndani kwa Peniela” akasema Mathew
“ What are we going to do Mathew.Are you sure Elibariki is ok?Nina wasi wasi sana na maisha yake” Akasema Anitha ambye alikuwa na wasi wasi mwingi.
“ Ngoja nijaribu kuwasiliana na Peniela anifahamishe kuna kitu gani kinaendelea” akasema Mathew na kuchukua simu yake akazitafuta namba za simu za peniela akapiga.Simu ikaita bila kupokelewa.
“ Mbona hapokei simu? Akauliza Mathew.
“ jaribu kupiga tena” akasema anitha.mathew akapiga tena na simu ikaendelea kuita.
Peniela akiwa katikati ya mzunguko akimpagawisha Dr Joshua simu yake ikaita lakini akaipuuzia.Ilipoita mara ya pili ikamlazimu kuakatisha mzunguko na kwenda kuipokea.Hakuzifahamu namba zile zilizompigia ni za nani akabonyeza kitufe cha kupokelea simu
“ hallow ‘ akasema
“ hallow Peniela? Akauliza Mathew
‘ Ndiyo,naongea na nani? Akauliza Peniela
“ unaongea na Mathew,rafiki wa jaji Elibariki”
“ Unasemaje? Akauliza Peniela
“ Hapa nyumbani kwako kuna askari wako getini na inaonekama wanajadiliana namna ya kuweza kuingia ndani.Kuna kitu gani kinachoendelea hapa kwako? Elibariki ni mzima?
“ Nyumbani kwangu? !!..peniela akashangaa
“ Ndiyo .” akajibu mathew na kumchanganya peniela.
“ pemiela wewe uko wapi? Uko ndani? Akauliza Mathew
“ hapana nimetoka sipo nyumbani”
“ Elibariki yuko wapi? Yuko ndani?
“ Ndiyo .Mathew naomba unisubiri kidogo niangalie namna ya kufanya” akasema Peniela halafu akamfuata Dr Jshua
“ peniela kuna nini? Mbona umebadilika ghafla? Akauliza Dr Joshua ambaye jasho liliendelea kumtiririka
‘ Dr Joshua nina tatizo limetokea na ninanahitaji msaada wako wa haraka”
“ Una tatizo gani peniela? Hebu naomba utulie na unieleze vizuri nini kimetokea? Akasema Dr Joshua.Peniela akamtazama kwa makini na kusema
“ Dr Joshua hivi tunavyoongea nyumba yangu imezingirwa a askari na wanataka kuingia nyumbani kwangu.Sielewi wanachokitafuta nini .Tafadhali Dr Joshua naomba unisaidie.Wewe una amri juu ya majeshi yote naomba uwaamuru waondoke pale nyumbani kwangu mara moja” akasema Peniela.DrJoshau akainama akafikiri kwa muda halafu akasema
“ Kuna kitu gani wanakitafuta pale kwako? Kuna kitu chochote ambacho kinaweza kusababisha wakafika pale kwako usiku huu?
“ Sina kitu chochote cha kuwafanya wafike pale kwangu usiku huu.Maisha yangu unayafahamu sina tatizo na mtu yeyote sasa kwa nini wakaizingira nyumba yangu kana kwamba ninauza dawa za kulevya? Tafadhali naomba uwaondoe pale kwangu mara moja” akasema Peniela.
“ Ok penny consider it done “ akajibu Dr Joshua na kuinuka akajifunga taulo na kuvaa fulana halafu akaufungua mlango .Walinzi wawili walikuwa wamesimama hatua chache toka chumba kile akawaita na kuongea na mmoja wao halafu akarejea tena chumbani.Baada ya sekunde kadhaa mlango ukagongwa akenda kuufungua
“ Mzee tayari kamanda wa kanda maalum yuko hewani.” Akasema yule mlinzi na kumpatia simu Dr Joshua
“ hallow Kamishna habari za usiku huu.samahani kwa kukusumbua” akasema Dr Joshua
“ Bila samahani mzee.” Akajibu Mkuu wa polisi kanda maalum ya dare s salaam
“ Nimekupigia kuomba msaada wako.” Akasema Dr Joshua
“ Ndiyo mzee nakusikiliza”
“ Kuna vijana wako muda huu wameizingira nyumba ya binti mmoja anaitwa Peniela una taarifa hizo?
“ Ndiyo mzee ninazo taarifa hizo”
“ Kuna nini hapo katika hiyo nyumba hadi izingirwe?
“ Mzee ,tumepokea taarifa kwamba Jaji Elibariki ambaye tumekuwa tukimtafuta ili kufahamu yuko wapi,amenonekana ndani ya ile nyumba na ndiyo maana vijana wangu wamekwenda pale ili kumkomboa kwani tuna hisi lazima atakuwa ametekwa nyara.”
“ Mna hakika na taarifa hizo za kuonekana kwa jaji Elibariki mahala pale?
“ Chanzo kilichotoa taarifa hizo ni chanzo cha ukakika ,ni mtu wa karibu wa peniela ambaye ni wakili aliyemsimamia kesi yake na akashinda.Mtu kama yule hawezi kutoa taarifa za uongo”
“Ok kamishna nimekuelewa lakini kuna jambo ninaliomba,naomba uwaondoe vijana wako kwa usiku huu na kesho zifanyike taratibu za kawaida za kufanya upekuzi katika nyumba ileili kubaini kam Elibariki yumo humo ndani au hayumo.Naomba unisaidie sana kwa hilo “
“sawa mkuu nitafanya hivyo.Nitawaondoa vijana wangu toka pale sasa hivi”
“Ahsante sana kamishna” akasema Dr Joshua na kukata simu
“ tayari .Kila kitu kimemalizika lakini naomba uniweke wazi Peniela ,kamishna wa kana maalum ya Dar es salaam anadai kwamba jaji Elibariki ameonekana nyumbani kwako.Hizi ni taarifa za kweli?
“ Elibariki ?! Peniela akashangaa
“ Ndiyo.Niliyekuwa nikongea naye ni kamanda wa kanda maalum ya kipolisi dare s salaam anasema kwamba askari wameizingira nyumba yako baada ya kupata taarifa za kuonekana jaji Elibariki nyumbani kwako.Taarifa hizi ni za kweli? Akauliza Dr Joshua.Peniela akamtazama na kusema
“ Do you trust them? Do you trust what they say?
“ Peniela niambie si kweli na nitakuamini”
“ Ahsante sana kwa kuniami Dr Joshua.Mimi sina mahusiano yoyote na Elibariki na wala hawezi kuja kujificha kwangu.Aliyewapa taarifa hizi atakuwa amewadanganya”
“Lakini inasemekana taarifa hizi zimetoka kwa mtu wako wa karibu sana.wakili wako aliyekuwa akikutetea katika kesi yako”
“ Jason? ! peniela akashangaa
“ Sifahamu kama ni huyo ama vipi lakini ndiye aliyetoa taarifa hizo polisi kwamba Elibariki yuko pale kwako.”
Peniela alipatwa na mshangao mkubwa sana kwa kusikia kwamba ni Jason ndiye aliyetoa taarifa zile kwa polisi.Haraka haraka akaanza kuvaa nguo zake
“ Kuna nini Peneila? Mbona unavaa nguo?
“ nataka nikaonane na Jason.kwa nini anifanyie hivi? Kwa nini anisingizie jambo zito kama hili?
“ Hakuna haja peniela jambo hili limekwisha malizika.Hakuna mtu atakaye ingia pale kwako.Mimi ndiye mkuu wa majeshi yote na kauli yangu ni ya mwisho kwa hiyo naomba utulize hasira tuendelee na mambo yetu” akasema Dr Joshua
“ hapana Dr Joshua .Siwezi kuendelea tena.Akili yangu imekwisha tibuka.usijali tutaonana tena siku yoyote ukiwa na nafasi.” Akasema na kumbusu Dr Joshua halafu akatoka kwa kasi akamuacha Dr Joshua akishangaa.
Peniela akaingia garini na kuondoka kwa kasi.Akiwa barabarani akapunguza mwendo wa gari na kuegesha pembeni akachukua simu yake na kumpigia Mathew
“ Mathew bado uko karibu na nyumbani kwangu?
“ Ndiyo niko hapa karibu na kwako”
“ Nini knaendelea hapo? Askari wamekwisha ingia ndani?
“ Hapana nimeshangaa wameingia katika magari yao na kuondoka”
Peniela kashusha pumzi
“ Ahsante Mungu.Dah ! hakuna siku niliyowahi kuogopa kama leo” akawaza Peniela na kuwasha gari lake akaendelea na safari
“ Mathew ninakuja niko njiani.tafadhali naomba usiondoke” akasema Peniela
“ Jason amefahamuje kama Elibariki yuko pale kwangu? Kwa nini akaenda kutoa taarifa polisi? Nadhani lengo lake ni kunikomoa mimi na Elibariki.Alijidanganya sana.Hakujua kama nina uwezo mkubwa zaidi yake.Nilikuwa na muheshimu sana na ,kumuona kama rafiki wa kweli lakini kumbe ni kijana ambaye hana akili hata moja.Nimemdharau sana na sitaki tena mahusiano naye na akiendelea kunifuatilia atakuwa ametangaza vita na mimi na nitamfunza adabu.” Akawaza Peniela
“ kwa sasa baada ya Elibariki kugundulika yuko pale kwangu lazima nimuhamishe.lazima nitafute mahala ambako nitakaa naye kwa raha mustarehe.sitaki nikae naye mbali .Tayari amekwiha niingia katika kila mshipa wa mwili wangu” akawaza Peniela
TUKUTANE SEHEMUJAYO…
No comments
Post a Comment