PENIELA (Season 1 Ep 29)

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Kwa nini unataka kufahamu kilichomuua Dr Flora? Wewe ni nani?

“Huna haja ya kufahamu mimi ni nani na kwa nini ninataka kufahamu kilichomuua Dr Flora ,nataka kusikia jibu moja tu ,utafanya au hutafanya?

Adolf akafikri kidogo na kusema

“ ok I’ll do it.Lakini kwa sharti moja “

“ Sharti gani hilo?

“ Hii iwe ni mara ya kwanza na ya mwisho kunitaka nikufanyie kitu cha namna hii.After this we’re done.Sitaki unibughudhi tena.Ukithubutu kunifuata tena I swear I’ll kill you.Do we have a deal?

“ deal “akasema Mathew.

“ Ok itanilazimu vile vile kuwataarifu baadhi ya madaktari ambao nitafanya nao uchunguzi huo siwezi kufanya peke yangu”

“ Huna haja ya kufanya hivyo.Tunaye daktari wetu ambaye utashirikiana naye kufanya huo uchunguzi.”

“ Yuko wapi huyo daktari?

“ Usijali utamuona tu.Twende tuondoke” akasema Mathew.Anitha alikwisha rejea garini akimsubiri Mathew,wakaingia garini na kuondoka.

ENDELEA………………………………………………….

Tayari jua limezama na kiza kimechukua nafasi yake.Watu walikuwa wengi sana katika makazi ya rais kuliko na msiba wa Dr Flora Joshua mke wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.Karibu viongozi wote wa serikali walikuwepo katika eneo hili la msiba na hivyo kulifanya eneo hili kuwa na ulinzi mkali mno.Kila aliyeingia mahala hapa alikaguliwa kwa kutumia mitambo maalum ili kuhakikisha kwamba hakuna anayeingia na silaha wala kitu kingine chochote cha hatari.Jaji Elibariki alikuwa katika pilika pilika nyingi akiwa kama sehemu ya familia ya rais.Kila mara alikuwa akiitazama saa yake ya mkononi na ilipotimu saa moja na nusu akampigia simu mkewe na kumuomba waonane.

“ Flaviana,nimeona nikufahamishe kwamba ninatoka kidogo ninakwenda kushughulikia lile suala.” Akasema jaji Elibariki

“ Ahsante sana Eli.Umefikia wapi mpaka hivi sasa kuhusu suala hili kwa sababu kwa mujibu wa ratiba mazishi ni kesho” akasema Flaviana

“ Siwezi kukupa jibu kwa sasa ila nitakaporejea nitakuwa na jibu la kukupa”

“ Ok My love,nakutakia kila la heri ila tafadhali kuwa makini sana” akasema Flaviana na kumkumbatia mumewe akambusu. Jaji Elibariki akaingia garini na kuondoka .Licha ya kuwa na mawazo mengi lakini kichwani kulikuwa na picha moja tu iliyokuwa imetawala,picha ya msichana mrembo ,mwenye uzuri usio na mfano,Peniela.

“ Ama kweli Peniela ameichanganya akili yangu sana kiasi kwamba nashindwa hata kukaa msibani.Kila dakika picha yake inanijia kichwani.Dah ! sikuwahi kuchanganywa na mtoto wa kike kiasi hiki.Sijui Yule msichana anatumia nini kiasi cha kuifanya akili yangu imuwaze yeye tu kila dakika.” akawaza Jaji Elibariki akiendelea na safari yake ya kuelekea kwa Peniela.

“ Ngoja nimpigie simu nimtaarifu kwamba niko njiani ninakwenda kwake” akapunguza mwendo wa gari na kuzitafuta namba za simu za Penny akampigia

“ Hallow Elibariki” ikasema sauti tamu ya Penny baada ya kupokea simu

“ Hallow Peniela,hujambo mtoto mzuri?

“Sijambo Elibariki,unaendeleaje?

“ Ninaendelea vizuri sana .Unafanya nini hivi sasa?

“ Nimejilaza hapa kitandani,akili yangu yote inakuwaza wewe tu.Ninakusubiri kwa hamu sana Elibariki.Mchana ulinionjesha kidogo nataka tuendelee pale tulipoachia .Bado uko msibani? Akasema Penny kwa sauti laini na kuufanya mwili wote wa Elibariki kusisimka.

“ Niko njiani ninakuja.Ndani ya dakika kumi na tano au ishirini nitakuwa nimefika.Hata mimi nina hamu sana na wewe.Kutwa nzima nimekuwa nikikuwaza wewe tu” akasema Elibariki

“ Ok Elibariki ninakusubiri.” Akajibu Penny na kukata simu

“ Dah ! huyu mtoto sijui ana kitu gani jamani ,kwa sababu kuongea naye tu hadi mwili wote umenisisimka.Anajua kumchanganya mwanaume.Vitu alivyonifanyia mchana sijawahi kufanyiwa na mwanamke yeyote Yule.hata mke wangu hajawahi kunifanyia mambo kama aliyonifanyia Penny.Sasa nimegundua kumbe wanawake nao wanaweza kuchangia sana ndoa zao kuporomoka.Kama mwanamke anashindwa kumfanyia mume wake mambo yanayoweza kumchanganya na badala yake anafanya mambo kwa mazoea tu,siku huyo mwanaume akikutana na mwanamke kama Peniela,mwenye kuyajua mambo,mwenye kufahamu nini mwanaume anahitaji,hiyo ndoa haitabaki salama.Lazima isambaratike “ akaendelea kuwaza Elibariki huku akikumbuka mambo aliyoyafanya na Peniela mchana wa siku hiyo.

Jaji Elibariki aliwasili nyumbani kwa Peniela ,akapiga honi na Penny akaenda kumfungulia geti.Usiku huu Penny alikuwa amevaa gauni fupi la kulalia lililokuwa likionyesha kila kitu cha ndani.jaji Elibariki alipomuona alipandwa na midadi.Tayari ikulu kulikwisha chachamaa.

“ karibu sana Elibariki” akasema Penny na kumkumbatia halafu akampiga busu zito na mkono mmoja ukashuka chini maeneo ya ikulu na kumfanya jaji Elibariki aanze kuvuta pumzi kwa kasi.Mapigo ya moyo yalibadika.Penny akamuongoza Elibariki hadi katika sofa sebuleni.

“ I missed you a lot Elibariki.Umenifanya nikuwaze kila dakika kwa mambo uliyonifanyia mchana.Please naomba kwanza unikate kiu yangu .” akasema Peniela kwa sauti laini ya kimahaba iliyozidi kumchanganya Elibariki

“ I need to take a shower first ” akasema Elibariki.Penny akambusu na kumshika mkono akamuongoza kuelekea bafuni .Wakati Elibariki akioga Penny akachukua simu yake akaenda sebuleni na kumpigia simu Jason na kuongea kwa sauti ya chini.

“ Hallo Penny.How are you my queen’ akasema Jason baada ya kupokea simu

“ I’m ok Jason.Uko wapi?

“Niko nyumbani.Uko wapi Penny mbona unaonekana kama una wasi wasi sana?

“ Ndiyo Jason.Nina wasiwasi sana.Kuna mtu yuko hapa kwangu ,ambaye amekuwa akinitaka kimapenzi kwa siku nyingi lakini nimekuwa nikimkatalia leo amekuja kwangu na anasema kwamba ameshindwa kuvumilia kuteseka kila siku kwa ajili yangu.Nina wasi wasi ana lengo baya.Please hurry up Jason.Sina amani hapa mtu huyu anaweza kunibaka” akasema Penny

“Ok Penny,ninakuja hapo sasa hivi.Kuna haja ya kuja na askari?

“ hapana hakuna haja ya kuja na askari. Nataka uje sasa hivi ili nimuonyeshe kwamba nina mpenzi wangu.Please hurry” akasema penny

“ Ok penny I’m on the way” akasema Jason .Penny akatabasamu

“ Kila kitu kimekwenda kama ninavyotaka.Ninachosubiri ni bomu tu kulipuka.Nataka Jason na Elibariki wachukiane wao kwa wao ili mpango wao wa kuchunguza kifo cha Edson usiendelee.Wakigombana hakuna kitakachoendelea.Nasikitika kufanya hivi kwani nitawakosa wote lakini ni kwa faida yao wenyewe.Jambo wanalotaka kulichunguza ni la hatari kubwa na hakuna namna ninayoweza kuwafanya wakaachana nalo zaidi ya kutumia njia hii.” Akawaza Penny.

“ Inaniuma sana kumkosa Jason,kwani ni mwanaume ambaye sina hakika kama nitampata kama yeye.Najutia kuingia katika maisha kama haya.Ninapata kila kitu ninachohitaji lakini siko kama wanawake wengine.Siwezi kuwa na maisha kama waliyonayo wengine.Lakini nitaendela na maisha haya mpaka lini? “akajiuliza Penny na mara akatokea Elibariki akiwa amejifunga taulo .Penny akaiweka simu mezani na kwenda kumkumbatia akaanza kumporomoshea mabusu mfululizo.Jaji Elibariki naye akajibu mapigo ,akamuinua Penny na kumpeleka sofani na kuanza kumshughulikia.

Mpambano ulikuwa mkali sana.walihama kabisa katika ulimwengu huu na kuhamia katika sayari nyingine kabisa yenye raha zisizoelezeka.Kilio na miguno kuashiria raha waliyoipata ndivyo vilivyokuwa vikisika.

Wakati Penny na jaji Elibariki wakijivinjari katika sayari ya mahaba,Jason alikuwa akiendesha gari kwa kasi ya aina yake kuwahi nyumbani kwa Penny.Maneno aliyoambiwa na Penny yalimstua sana.Alitamani apate na kufika mara moja nyumbani kwa Penny ili amfundishe adabu mwanaume huyo ambaye yuko nyumbani kwa penny kwa lengo la kufanya mapenzi.

“ Leo nataka nimfundishe adabu huyo bazazi ambaye anapenda kuvamia wanawake wa watu.Haelewi ni kiasi gani nimewekeza hadi kumfanya Penny awepo hapa alipo sasa hivi. I’ve sacrificed a lot for her.Siwezi kuruhusu mwanaume mwingine aje na kuanza kufanya mambo ya kipuuzi kwa mwanamke ambaye ninategemea awe mke wangu.” Akawaza Jason akiwa na hasira nyingi.

Alifika nyumbani kwa Penny akasimamisha gari nje akashuka na kufungua mlango mdogo wa geti ambao haukuwa umefungwa,akaingia ndani.Kitu cha kwanza kukiona ni gari alilolifahamu .

“ Elibariki!!..akasema kwa mshangao

“Hili ni gari la Elibariki.Anatafuta nini hapa kwa penny? Yawezekana labda Penny amempigia ili kuomba msaada” akawaza Jason na kupiga hatua ndefu kuelekea ndani.Akaufikia mlango wa sebuleni na kusimama,akajaribu kusikia sauti za watu lakini ni muziki tu ndio uliokuwa ukisikika.Akakinyonga kitasa mlango ukafunguka akaingia ndani .Akapiga hatua tani akakivuka kichumba kidogo na kuingia sebuleni.Alitamani ingekuwa ni ndoto lakini haikuwa ndoto bali ni kitu cha kweli alichokuwa akikiona mbele yake.Alipatwa na mstuko mkubwa na kuhisi miguu yake inaisha nguvu akaegemea ukuta.Mwili wote ulikuwa unamtetemeka.Katika sofa jaji Elibariki na Peniela walikuwa wakifanya mapenzi.Mwili wote ukamtetemeka kwa hasira

“ Elibariki !!!...akaita kwa hasira Jason.Jaji Elibariki akastuliwa na sauti ya Jason akageuka ghafla na kukutana na sura iliyojaa hasira

“ Jason !!!..akasema jaji Elibariki kwa mshangao mkubwa.Hakuwa akitegemea kumuona Jason maeneo yale mida ile

“ What are you doing here Jason? Akauliza Elibariki kwa mshangao huku jasho likimtiririka.

“ What are you doing here Elibariki? Akauliza Jason kwa hasira.Elibariki akasimama

“ Nakuuliza Elibariki unafanya nini hapa na mpenzi wangu? Akauliza Jason kwa hasira huku akimsogelea Elibariki

“ Mpenzi wako? Toka lini Peniela akawa mpenzi wako? Huyu ni mwanamke wangu.Nashangaa ulivyokosa adabu na kuingia katika nyumba za watu bila kubisha hodi.” Akasema kwa ukali jaji Elibariki

“ Peniela is your woman? Akauliza Jason kwa hasira

“ Peniela is your woman?akauliza tena Jason

“ Is she your woman? Jaji Elibariki naye akauliza

“ Nakuuliza Jason Peniela ni mwanamke wako? Akauliza Elibariki huku naye hasira ikizidi kumpanda.

“ Yes Peniela ni mwanamke wangu…”

“ You are idiot!! ..akasema Elibariki .Kauli ile ikamkasirisha sana Jason na kufumba na kufumbua akarusha ngumi nzito iliyompata Elibariki shavuni akaanguka chini.Vurugu kubwa likaibuka mle sebuleni.Penny akaogopa sana kwa namna walivyokuwa wakirushiana makonde. Wakati wakiendelea kupigana,Jason akachukua chupa ya mvinyo na kumpiga nayo Elibariki kichwani, akaanguka na kupoteza fahamu.Peniela alikuwa amejificha katika pembe ya sebule akitetemeka.Baada ya Jaji Elibariki kuanguka chini huku damu zikimtoka Jason akaogopa na kudhani ameua,akatoka mbio.Penny akamkimbilia Elibariki pale chini .Aliogopa sana .Alichanganyikiwa na hakujua afanye nini.Mara mle sebuleni wakaingia watu watatu.



“ Hello Penny.Nini kimetokea hapa? Akauliza mmoja wa wale jamaa.Penny hakuweza kujieleza,alikuwa amechanganyikiwa .Mmoja wa wale jamaa akaliokota taulo akamfunika kwani alikuwa bado mtupu,halafu akamshika mkono na kumuinua

“ Its ok Penny.Go to your room and wash yourself.We’re going to take care of this” akasema Yule jamaa aliyekuwa akiongea kwa upole.Akamsindikiza Penny hadi chumbani kwake halafu akarejea sebuleni .Penny akakaa kitandani alikuwa akitetemeka.Picha ya tukio lile ilimuogopesha sana.

“ Sikutegemea kama jambo hili lingekuwa baya kiasi hiki.Nimeogopa sana.Wale wanaume karibu wangetoana roho mbele yangu.lakini nashukuru kwa kufanikiwa kuwavuruga.Kwa sasa mipango yao yote imevurugika.Nim

ewakosa wote wawili lakini watakuwa salama.Walikokuwa wakielekea si kuzuri hata kidogo.” Akawaza Penny

“ Nimefanya ulaghai mkubwa sana.Nimecheza na akili za watu.Niwamedanganya kwa mapenzi na wakadanganyika.They are all going to hate me.I’m a monster.” Akawaza halafu akaingia bafuni kuoga

“ Watu wale walioingia ghafla pale ndani ni akina nani? Wametoka wapi? Wamenifahamu vipi? Sina hakika kama nimewahi kukutana nao sehemu yoyote.Yawezekana ni wale wale jamaa waliokuja kupekua nyumba yangu wakati sipo.” akajiuliza Penny.

Watu wale watatu walimpatia Jaji Elibariki huduma ya kwanza na kuizuia damu isiendelee kumwagika.Alipozinduka alihisi maumivu makali mno hasa sehemu za kichwani.Mmoja wa wale jamaa akamfuata Penny chumbani kwake na kumgongea.Penny akafungua mlango

“ Penny mtu wako amezinduka na tayari tumezuia damu isiendelee kumwagika.Vijana wangu watanmpeleka hospitali ili akapatiwe matibabu na kushonwa jeraha lake.Hatuna haja ya kufahamu klilichotokea kwani hayo ni mambo yako binafsi lakini tuko hapa kukuchukua na kukupeleka mahala unakojitajika usiku huu. “ akasema Yule jamaa

“ Nyie ni akina nani? Akauliza Penny

“ 0065 “ akasema Yule jamaa na Penny akawa ameelewa ni akina nani.

Penny hakusema kitu akatoka mle chumbani na kuelekea sebuleni.Alisikitika sana kwa kumuona jaji Elibariki akiwa katika hali ile.Hakutaka kuongea naye chochote,vijana wawili wakambeba Elibariki na kumpakia katika gari lao .

“ Penny ,tutahakikisha mtu wako anapatiwa matibabu yenye uhakika na anakuwa salama” akasema Yule jamaa ambaye hakutaka kujitambulisha jina lake

“ Nitashukuru sana.hakikisheni tafadhali anapatiwa huduma ya uhakika” akasema Penny akaingia katika gari lingine na Yule jamaa wakaondoka.Jaji Elibarii akapelekwa hospitali

********

Saa na nne na dakika nane,Mathew,Anitha,na Dr Michael ,wakiongozwa na kanali Adolf wakawasili katikahospitali kuu ya jeshi wakitumia gari la Kanal Adolf ambalo halikukaguliwa getini.Baadakushuka walielekea moja kwa moja katika ofisi ya kanali Adolf ambako walivaa makoti meupe ya kidaktarina kisha wakaanza kuelekea katika chumba cha kuhifadhia maiti.Haikuwa kawaida kwa chumba hiki kulindwa ,lakini toka mwili wa Dr Flora ulipoletwa katika chumba hiki kumekuwa na ulinzi mkali.

Kanali Adolf akajitambulisha kwa wale wanajeshi wawili waliokuwa wakilinda usalama wa chumba kile cha maiti halafu wakaingia ndani .Kwa usiku huu ndani ya chumba kile kulikuwa na wafanyakazi wawili tu.Wote wanamfahamu kanali Adolf na walipomuona wakamsalimu kwa heshima .Akamuita mmoja akamuagiza aupeleke mwili wa Dr Flora katika chumba cha kufanyia uchunguzi wa maiti haraka sana.Ndani ya dakika tano tayari mwili ukaletwa na kulazwa juu ya kitanda.Kwa pamoja Kanali Adolf na Dr Michael wakaaanza kuufanyia uchunguzi huku Mathew na Anitha wakiwa katika tahadhari kubwa sana.

*********

Penny hakujua anapelekwa wapi na hakutaka kuhoji ili kufahamu anapelekwa wapi.Akili yake yote ilkuwa ikiwaza kuhusu tukio lililotokea usiku huo .Picha ya Jason na jaji Elibariki wakipigana ikamrudia na kumtoa machozi.

“ Nimefanya mambo mengi mabaya lakini hili la leo limenisikitisha sana.Nmeumia sana.Nimewaumiza watu walionipenda na kunipigania. Kwa sababu yangu wanaume wale watajenga uadui mkubwa kati yao na sina hakika kama suala hili litaishia pale,lazima litaendelea.Lazima kutakuwa na uhasama mkubwa mno.Lakini Kwa upande mwingine nimewasaidia kutokujiingiza katika matatizo kwa kitu cha hatari walichotaka kukifanya.Mpango wa kuchunguza kifo cha Edson umeisha” Akawaza penny

Safari ilikuwa ya kimya kimya namuda mwingi penny alikuwa ameinama huku mkononi mwake akiwa na kitambaa cha kufutia machozi yaliyokuwa yakimchuruzika kila alipokumbuka picha ya ugomvi ule.

Hatimaye walikata kona na kuingia katika jumba moja kubwa la ghorofa zipatazo nne lililozungukwa na miti mingi.Magari zaidi ya ishirini yalikuwa yameegeshwa katika maegesho kubwa iliyokuwamo ndani ya jumba hili.Kijana mmoja aliyevaa suti nyeusi akafika na kumfungulia mkono Penny na bila kujitambulisha akamuomba amfuate.Penny aliendelea kujiuliza mahala pale ni wapi .Akaendelea kumfuata yule kijana wakaanza kupanda juu ghorofani hadi walipofika ghorofa ya nne.Kote walikopita walikutana na watu kadhaa na wote wakiwa wamevalia suti.Kila mmoja alionyesha heshima kubwa kwa Peniela na kuzidi kumshangaza.Hakuwahi kufika mahala pale wala hakuna aliyemfahamu lakini wao walionekana kumfahamu na kumuheshimu sana.

“ Nimeletwa hapa kufanya nini? Mbona kila mtu ninayekutana naye anatoa heshima kubwa? Akajiuliza na mara Yule kijana aliyeongozana naye akasimama akaongea na mtu mmoja hivi pande la mtu.Mtu Yule akamsalimu penny kwa heshima kubwa halafu akamuomba amfuate.Penny akazidi kushangaa.

UCHUNGUZI WA KIFO CHA DR FROLA UMEANZA ,JE WATAFANIKIWA KUGUNDUA CHANZO CHA KIFO CHAKE? PENIELA AMEPELKWA WAPI? …MPENZI MSOMAJI TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO

No comments

Featured post

MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI

 MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI 1.Kuhudumiwa na Mtu anaye SMILES. Humfanya mteja ajihisi yuko huru zaidi kuuliza na kuamini unaweza k...