PENIELA (Season 1 Ep 11)

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Toka nimezaliwa hata baba yangu hajawahi kunipiga kofi sembuse wewe ng’ombe ! ..Kauli ile ikampandisha hasira Elibariki na kuanza kumshushia mke wake kipigo kikali kilichomfanya apige ukelele mkubwa .Jaji Elibariki hakujali kelele zile akaendelea kumpa kipigo mkewe.Hadi anamuachia Flaviana alikuwa anavuja damu.

“ Siku nyingine usithubutu kabisa kunidharau paka wewe ..! akasema jaji Elibariki huku akitweta kwa hasira Huku akilia,Flaviana akaingia bafuni na kujifuta damu zilizotoka katika majeraha yaliyotokana na kipigo kikali

“ Eli umenipiga hadi kunitoa damu.Sasa nitakuonyesha mimi na wewe nani mwenye nguvu.I swear in heaven and earth lazima nikuonyeshe kazi na hautanisahau mpaka unaingia kaburini”akasema kwa hasira flaviana na kutoka kwa kasi akaingia katika gari lake na kuondoka kwa kasi

“ Nimechoshwa na dharau za familia hii.Yote hii ni kwa sababu baba yao ni rais .Hapana hawawezi kunitisha hata kidogo,hakuna aliye juu ya sheria.” Akasema jaji Elibariki kwa hasira.

ENDELEA…………………………

Jaji Elibariki alikaa kitandani na kuanza kutafakari maisha yaketoka alipokutanana Flaviana ,wakapendana,wakwa wachumbanabaadae wakafungandoa.Aliyatafakari maisha yake ya ndoa toka walipooana hadi leo hii

“ Sina hakika kama tuliingia katika ndoa tukiwa tumejiandaa vya kutosha.Sina hakika kama tulikuwa na mapenzi ya kweli au zilikuwa ni tama tu za ujana.Toka tumeyaanza maisha yandoa hakuna amanindani mwetu.It’s been a living hell to me.Tukiwa nje tunaonekana ni watu wenye mapenzi mazito lakini hajuna ajuaye siri yetu ya ndani.Maisha yetu yamejaa mifarakano,dharauna ugomvi.Nimechoshwa na maisha haya.Nimechoka kuwadanganya watu kwamba tunapendana kwa dhati wakati si kweli.Nadhani ni wakati muafaka sasa wa kufanya maamuzi na kila mmoja wetu akatafute furaha ya maisha yake.Siwezi kuendelea na maisha kama haya” akawaza halafu akaenda katika kabati dogo lililokuwa mle chumbani akalifunguana kutoa chupa ya mvinyo akajimiminia katika glasi akanywa na mara sura a Peny ikamjia kichwani “ Penny !!..akasema kwa sauti ndogo huku akitabaamu

“ Mwanamke kama Penny anafaa sana kuwa mke.Aba uzuri wa kipekee ambao sioniwa kumfaanisha naye na ana adabu na hata ukiongea naye utabaini wazi kwamba ni mwanamke mqwnye heshima kubwa/Jaji Elibarikiakaendelea kuwaza na mara akastuliwa namlio wa simu.Akaichukuana kutazmaa mpigaji ,alikuwa ni baba mkwe wake Dr Joshua,rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.



“ Kazi imeanza” akasema kimoyo moyo na kubonyeza kitufe cha kupokelea simu

“ Hallo mzee shikamoo”

“ Marahaba mheshimiwa jaji,habari za kwenu?

“ Habari nzuri tu mzee,sijui ninyi huko”

“ Sisi wazima.Eli uko wapi?

“ Niko nyumbani mzee”

“ Ok vizuri.Nakuomba hapa ikulu sasa hivi nina maongezi nawe” akasema Dr Joshua na kukata simu

“ Flaviana amekwenda kunishitaki kwa baba yake akidhani labda nitamuogopa.Sintomuogopa mtu yeyote hata kama ni rais wan chi.Kuanzia sasa yeyote atakayenidharau kwa namna yeyote ile nitapambananaye” akawaza huku akivaa koti na kutoka kueleka ikulu kuonana na baba mkwe wake. Ilimchukua dakika zaidi ya hamsini kuwasili katikamakazi ya rais.Baada ya kama dakika kumi na tatu toka awasili ,Dr Joshua akajitokeza sebuleni.Jaji Elibariki akasimama wakasalimiana “ Mheshimiwa jaji ,hebu nieleze nini kimetokea huko kwenu na kusababisha umpige mwenzako na kumuumiza kiasi kile? Akaanzisha mazungumzo Dr Joshua.Elibariki akavuta pumzi ndefu na kisha akamsimulia rais kila kitu kilichotokea na kusababisha apandwe na hasira na kumpiga mkewe.

“ Nimekuelewa Elibariki ,lakini pamoja na yote aliyoyafanya mwenzako ulitakiwa ujizuie, hukupaswa kufikia hatua ya kumpiga mwenzako namna ile.Migongano ndani ya nyumba ni kitu cha kawaida na suluhisho lake ni kukaa mkaongea mkayamaliza na si kurushiana makonde.Wewe kama kichwa cha nyumba unahitajika uwe na busara ya hali ya juu “ akasema Dr Joshua

“ Nakuelewa mzee,lakini nilifikia maamuzi ya kumpiga kidogo mke wangu kutokana na dharau alizoniletea.Kama nilivyokueleza mzee ni muda mrefu sasa amekuwa akinidharau sana na leo hii uvumilivu ulinishinda nikaona bora nimuonye kidogo” akasema Elibariki “ Siku nyingine endapo atakuletea dharau na kiburi,wasiliana nami moja kwa moja kabla ya kuchukua maamuzi ya kumpiga.Sipendi sana kuona mwanangu yeyote akilia machozi na hasa ya kupigwa na mwanaume” akasema Dr Joshua

“Lakini mzee, Flaviana ni mke wangu na mambo yetu yanndani tunayamaliza wenyewe.Haitapendeza kila siku niwe nakupigia simu na kukwambia kwamba mwanao amenidharau.Naomba mzee utuachie mambo yetu ya ndani tuyamalize sisi wenyewe.” Akasema Elibariki

“Kuyamaliza kwa staili hii ya kutoana damu? No !.. Sitaki kabisa mwanangu aguswe tena na kutolewa damu.Usinione ninaongea nawe hapa lakini nimechukizwa mno na kitendo ulichokifanya leo cha kumpiga mwanangu.Naomba kisijirudie tena.Marufuku kumfanya mwanangu sehemu ya mazoezi” akasema Dr Joshua kwa sauti ya juu yenye amri ndani yake .Jaji Elibariki akakereka sana kwa maneno yale ya baba mkwe wake

“ Lakini mzee………….” Akataka kusema jambo ,akazuiwa na Dr Joshua

“ Hakuna cha lakini…..Nimesema sitaki mwanangu aguswe and that’s fnal.Sitaki tena mjadala.Hata akikukosea vipi sitaki umpige.Nieleze mimi mwenyewe nitaongea naye” akasema kwa ukali Dr Joshua “ lakini mzee huyu ni mke wangu na amekuwa akinifanyia mambo mengi ya dharau ambayo siwezi hata kukueleza.Unapoongea maneno kama hayo unampa nguvu ya kufanya anachokitaka kwangu kwa kuwa anajua baba yake anamtetea” akalalamika Elibariki.Dr Joshau akasimama na kumsogelea “ I’m her father and I’m warning you….” Akasema Dr Joshua.maneno yale yakamkera sana Elibariki naye akasimama. “ Yes 1 you are her father but I’m her husband !!.... akasema Elibariki kwa sauti ya juu kidogo.

“ Elibariki,tafadhali chunga sana maneno unayoongea mbele yangu.Wewe bado hauna uwezo wa kusimama na kubishana na mimi.Ukumbuke kwamba ni mimi ndiye niliye kutoa huko maporini na kukupandisha hadi hapa ulipo.kwa hiyo kuwa makini sana siku nyingine unapoongea na mimi.Nina uwezo wa kukufanya chochote kile” akafoka dr Joshua.Elibariki akamtazama kwa macho makali na kusema

“ Naomba unisikilze mzee.Nimechoshwa na wewe na wanao kila mara kunisimanga kutokana na cheo hiki.Naomba mfahamu wewe na wanao kwamba cheo hiki hukunipa wewe bali nimepewa na Jamhuri ya muungano wa Tanzania na nimepewa kwa sababu ninafaa na nina vigezo vyote vya kuwepo hapa nilipo.Kwa maana hiyo naomba muache kuanzia sasa kunisakama kuhusiana na cheo hiki.Kitu kingine mnachotakiwa kukifahamu ni kwamba ofisi hii si mali ya familia,kwa hiyo si wewe wala wanao mnaoweza mkanishinikiza nifanye kazi yangu kwa matakwa yenu.Ninaifanya kazi yangu kwa mujibu wa sheria za nchi na si kwa kumfurahisha mtu Fulani..”akasema kwa ukali na kutoka kwa hasira akimuacha Dr Joshua akishangaa.

“ Nimemueleza ukweli wake,akichukia shauri lake,nimechoshwa na dharau zao” akawaza Elibariki huku akiingia katika gari lake na kuondoka

“ Kichwa changu kimevurugwa kabisa na Yule mzee.I need someone to talk to.I need some comfort” akawaza na mara sura ya penny ikamjia

“ penny !!... I need to talk to her.pengine kichwa changu kinaweza kutulia” akapunguza mwendo wa gari akatoa simu na kuzitafuta namba za Penny ,akapiga lakini haikuwa ikipatikana.

*********

Asubuhi na mapema jaji Elibariki aliamka na kufanya mazoezi ya viungo halafu akajianda na kuondoka.Flaviana hakurejea nyumbani usiku toka alipoondoka

“ Nadhani huu utakuwa ni mwanzo wa maisha mapya.Sina hakika kama kuna suluhu yoyote itapatikana tena baina yangu na Flaviana.Ni wakati sasa wa kuanza kuitafuta upya furaha ya moyo wangu ambayo nilitegemea kuipata kwa Flaviana lakini kumbe nilikuwa najidanganya.Nimeambulia karaha badala ya raha.Toka nilipomuoa hadi hivi leo hata mtoto amekataa kunizalia kwa kisingizo cha kutokuwa tayari.Hapana imetosha sasa.Maisha haya lazima yafikie mwisho.Kwa sasa ngoja kwanza nielekeze nguvu kumtafuta muuaji wa Edsoni ili Penny aweze kuwa salama” Mara tu alipomkumbuka Penny,akatabasamu na kutoa simu yake akazitafuta namba za Penny akapiga lakini bado simu yake haikuwa ikipatikana.

“ Ameamua kuizima simu yake,inawezekana hataki usumbufu toka kwa watu.Ametoka katika matatizo makubwa na anahitaji muda wa kukaa mwenyewe atafakari maisha yake bila usumbufu toka kwa watu” akawaza Jaji Elibariki Moja kwa moja alielekea Mandarini Hotel mahala ambako hupenda sana kwenda kupata kifungua kinywa.

“ Watu wengi wananishangaa ni kwa nini mtu kama mimi,Jaji wa Mahakam kuu ninakuja kupata kifungua kinywa hotelini? Hawajui Kero nilizonazo katika ndoa yangu.lakini soon mambo yote haya yatakwisha and I’ll be happy again.” Akawaza wakati akiendelea kupata kifungua kinywa. Toka Mandarin hotel,akaelekea ofisini kwake ambako hakukaa sana akatoka akaelekea mahala alikopanga akutane na Mathew.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…

No comments

Featured post

MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI

 MAMBO NANE YANAYOWAVUTIA WATEJA WENGI 1.Kuhudumiwa na Mtu anaye SMILES. Humfanya mteja ajihisi yuko huru zaidi kuuliza na kuamini unaweza k...