PENIELA (Season 1 Ep 7)
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Akiwa njiani kurejea nyumbani kwake ,Jaji Elibariki akampigia simu
“ Halo jaji” akasema Jason
“ Jason,umemfikisha penny salama?
“ Ndiyo nimemfikisha salama.
Niko njiani kuelekea nyumbani “
“ Ok Jason.Nimezungumza mambo mengi na Penny lakini kuna jambo moja nimeligundua toka kwake”
“ jambo gani Jaji?
“ Kuna kitu anakifahamu kuhusiana na kifo cha Edson lakini hayuko tayari kuliweka wazi”
“Are you sure? Akauliza Jason
“ yah ! I’m sure.Kuna kitu anakifahamu lakini hayuko wazi kukisema.”
“ sasa tutafanya nini?
“ Tutaendela na uchunguzi wetu kimya kmya bila ya kumshirikisha Penny.” Akasema Jaji Elibariki
Jason akafikiri na kusema
“ Ok Jaji.Tutaonana kesho na tutajadili kwa kirefu” akasema Jason na kukata simu
ENDELEA……………………….
Baada ya Jason kuondoka,Penny akaenda chumbani kwake akajitupa kitandani.Alionekana kuwa uso wenye tabasamu
“ Ni mara ya kwanza nimetoka out baada ya mwaka mzima.Wow it was wonderfull. Elibariki is real a gentleman. Nimefurahi sana kukaa meza moja naye.Nii mtu ambaye ndiye aliyenifanya niwe huru.Bila yeye kwa sasa ningekuwa gerezani maisha yangu yote au nikisubiri kunyongwa.Sintaweza kumsahahu katika maisha yangu.
Hata hivyo he’s so cute.Ni jaji kijana na mwenye moyo wa huruma” akawaza Penny huku akitabasamu lakini mara akabadilika na kuonekana kuwa na mawazo
“ Jason na Jaji Elibariki wanataka kujiingiza katika jambo la hatari kubwa.Suala la kifo cha Edson si suala rahisi kama wanavyolichukulia.Ni jambo zito na la hatari .Mjadala wake ulikwisha fungwa na hakuna tena uchunguzi wowote utakaofanyika tena.Natamani kuwaambia wasiendelee na kitu wanachotaka kukifanya lakini nashindwa.Ninachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kwamba hawafanikiwi katika usala hili na hivyo kukata tamaa na kuacha kabisa kuchimba undani wa kifo cha Edson.Hii itakuwa ni kwa ajili ya usalama wao wenyewe” Akawaza Penny na kustuliwa na mlio wa simu.
Akatazama mpigaji akakutana na namba ambazo hazikuwa na jina mara moja akawa amemtambua mpigaji. Akavuta pumzi ndefu halafu akabonyeza kitufe cha kupokelea
“ Hallow “ akasema kwa sauti ya uchovu.Sekunde kadhaa zikapita halafu sauti ya upande wa pili ikasema
“ Hallow Penny.How are you?
“ I’m fine.How are you? Akajibu Penny
Kimya kifupi ikapita tena na mtu Yule akauliza
“ Penny kwa nini umenifanyia dharau kubwa kama leo? Lini utaufungua moyo wako kwangu? Lini utakuwa tayari kukaa na kunisikiliza? Ikauliza sauti ile nzito iliyoongea kwa upole.Penny akashindwa kujibu
“ Kwa nini umeshindwa kuja kuonana nami kama tulivyokuwa tumepanga? Akauliza mtu Yule.Penny akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Mr President can we stop this?
“ Stop what ?
“ Mr President we can go on like this.Its time to end things now” akasema Penny
“ Penny ni hapo tu unaponiudhi “
“ Dr Joshu …” akataka kusema kitu Penny lakini Dr Joshua akamzuia
“ Don’t say anything Penny.You know exactly how much I love you and I’ll never stop loving you” akasema Dr Joshua kwa sauti yenye ukali kidogo.
“ Acha kunidanganya Dr Joshua !! “ Penny naye akasema kwa sauti yenye ukali kidogo ndani yake
“ Sikudanganyi Penny na sijawahi kukudanganya kwamba ninakupenda kwa moyo wangu wote.”
“ Liar !!..” akasema Penny
“ Kama unayoyasema yana ukweli usingekubali kuona nikitaka kuangamia.Unsingethubutu kuniona nikiozea gerezani na kunusurika kufungwa maisha wakati ukijua kabisa kwamba sikutenda lile kosa.Sikumuua Edson .Pamoja na kufahamu hilo lakini bado hukufanya lolote kunisaidia na badala yake ukakubali nibambikiwe kesi ile ili nikafungwe.You don’t love me at all” akasema Penny kwa hasira
“ Penny I love you.
real do.Najua hutaamini lakini fahamu kwamba niliumia kukuona ukiwa gerezani lakini nilishindwa namna ya kukusaidia kwa sababu kwa wakati ule bado ulikuwa umenikasirisha mno na nilitamani hata ufungwe gerezani ili nisikuone tena katika maisha yangu yote.Kitendo cha kuanzisha mahusiano na Yule kijana Edson kiliniumiza sana na ndiyo maana yakatokea yale yaliyotokea lengo likiwa ni kukufunza adabu kidogo ili uwe na heshima kwa watu wazima na wenye nguvu.” Akasema Dr Joshua .Penny akafuta machozi.Dr Joshua akaendelea
“ Penny naomba nikuweke wazi kwamba moyo wangu uliumia mno na kuvunjika pale ulipoingia katika mahusiano na yule kijana Edson na ukanisaliti na kwa sababu yako akamuacha hadi mwanangu Anna.Pamoja na yote yaliyotokea bado ninashindwa kukutoa moyoni mwangu.Bado nakuhitaji Penny katika maisha yangu.Ni wewe tu ambaye unaweza kunipa furaha ninayoihitaji.Tafadhali Penny naomba tuyasahau yote yaliyopita na tuufungue ukurasa mpya.”
Penny akafikiri kidogo na kusema
“ so you killed him !..” akasema Penny huku machozi yakimdondoka mashavuni
“.Yes I did.You are mine Penny,and mine alone.yeyote ambaye atataka kuchukua nafasi yangu kwako sintasita kumfanya kama nilivyomfanya Edson na ukumbuke kwamba siku ukifungua mdomo wako ndiyo utakuwa mwisho wako kwa hiyo basi …….” Dr Joshua akakatishwa na Penny ambaye machozi yalikuwa yanamtoka
“ You are a devil..!!” akasema Penny kwa ukali
“ Penny naomba unielewe kwamba nina kupenda na nitafanya kila linalowezekana ili mimi na wewe tuwe pamoja.My wife is sick and will die soon.Hawezi kunipatia kile ninachohitaji na ninachokipata toka kwako.She’ll die soon and you’ll be the first lady so please open your heart for me….” Akasema Dr Joshua
“ Dr Joshua,naomba hii iwe ni mara ya mwisho kunipigia simu.Wewe ni rais wa nchi na una mke wako wa ndoa kwa hiyo naomba uachane kabisa na mimi.Tafadhali angalia masuala makubwa ya nchi na mke wako mgonjwa.She needs you” akasema Penny
“ Penny kwa nini hutaki kunielewa? Nimekwisha kwambia kwamba hakuna kitu zaidi ya kifo kitakachoweza kunitenganisha na wewe.Nimekuchagua wewe tu na nitafanya kila niwezalo na nitatumia nguvu zote nilizonazo mpaka niwe nawe tena.Najua unanichukia sana kwa sasa lakini tutayamiliza mambo haya na tutakuwa wamoja tena. No woman will say no to me” akasema Dr Joshua.
Penny akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Let us have a deal Dr Joshua”
“ A deal !!..
“Yes a deal. I’ll keep my mouth shut.I’ll never tell anybody that its you who killed Edson and I’ll die with my secret if you’ll let me go”
“ hahaha Penny unanifurahisha sana.I’ll never let you go and you’ll keep your mouth shut because I did that for us,me and you.So we don’t have a deal.I know down deep in your heart that you do love me.”
“ I don’t love you Joshua and I’ll never love you”
“ Who do you love? Wakili wako Jason?
Au jaji Elibariki? Penny akastuka baada ya kutajiwa jina la Elibariki
“ So you are following me ?!! akauliza Penny
“ Penny ninafahamu kila hatua unayoipiga.Ninafahamu jioni hii umekataa mwaliko wangu na ukaenda kuonana na Jaji Elibariki.Be careful.Jaji Elibariki amemuoa mwanangu lakini sintosita kumuadhibu pale atakapoamua kuvuka mipaka na kumsaliti mwanangu kama Edson alivyomsaliti mwanangu Anna.”
Penny akahisi kuishiwa nguvu akashindwa aseme nini.
“ Penny nitakuwa na safari ya kwenda Arusha wiki ijayo kwa hiyo jiandae nawe utakwenda Arusha.Kareem atashughulikia kila kitu kuhusu safari hiyo.Kwa heri Penny” akasema Dr Joshua na kukata simu.Penny alihisi jasho likimchuruzika .
“ I’m back to a living hell.!..Nayachukia sana maisha haya lakini sina namna tena tayari nimenaswa.Endap
o nitaenda kinyume na huyu mzee kuna uwezekano yakanifika makubwa .Nimeponea chupu chupu kesi ya mauaji na safari hii lazima niwe makini sana kwa kila ninachokifanya.” akawaza Penny huku kijasho kikimchuruzika na mara simu yake ikaita,akatazama mpigani na kubonyeza kitufe cha kupokelea
“ Hallow” akasema
“ Penny don’t say No to Mr president.Fanya kila atakachokuamuru ufanye.We’re so close” ikasema sauti ile na kukata simu.Penny akahisi kuchanganyikiwa.
TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO
No comments
Post a Comment