PENIELA (Season 1 Ep 15)
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Jason alimfikisha Mathew nyumbani kwake na kisha akaendelea na safari ya kuelekea kwake.Mathew akaingia ndani mwake na kitu cha kwanza alichokifanya ni kuelekea katika chumba chake kikubwa kilichokuwa na runinga kubwa nane zilizotundikwa ukuitani.Akaziwasha runinga zote na zikaanza kuonyesha picha zikaanza kuonekana.
“ wow ! my birds are working” akasema na kukaa kitini akaanza kufuatilia picha zile zilizokuwa zikionekana katika runinga.Runinga namba sita ilikuwa ikionyesha makazi ya Peniela.Vifaa vile mithili ya vipepeo Mathew alivyoviweka katika nyumba ya Peniela vilikuwa ni kamera ambazo zilikuwa zikionyesha kila kilichokuwa kikiendelea katika makazi yale.Alizipeleka mbele picha zile na hakukuonekana mtu yeyote akiingia katika makazi yale hadi ilipotuimu saa mbili na dakika ishirni na mbili.Geti dogo lilifunguliwa na watu wawili wakaingia kwa kunyata huku akiwa na bastora mikononi.
“ Who are these people? Akajiuliza Mathew huku akiisogelea karibu runinga yake.
ENDELEA………………………………
Watu wale wawili walikuwa makini sana wakiangaza huku na huko halafu wakaweka kitu Fulani kidogo katika mlango wa kuingilia sebuleni kwa Penny.
“ Wanaweka nini pale? Akajiuliza Mathew na kuikuza picha ili aone kitu kile kilichokuwa kimewekwa pale mlangoni.
“ Kamera !..” akasema kwa sauti ndogo
“ Wameweka kamera .Kwa nini wameweka kamera mlangoni? These people looks so professional” akawaza Mathew.
Baada ya kuweka kamera ile mlangoni kwa Peniela,kwa kutumia vifaa maalum wakafungua mlango wakaingia ndani.Mathew hakuweza kuona kilichokuwa kinaendelea ndani kwa sababu hakuwa ametega kamera yoyote ndani ya nyumba ya Penny.Baada ya kama dakika kumi hivi watu wale wakatoka na kuondoka na kuzidi kumchanganya Mathew
“ Watu wale ni akina nani? Wamefuata nini kwa Peniela? Akaendelea kujiuliza Mathew.Akarudisha tena picha nyuma na kuwatazama vizuri watu wale
“ Watu hawa ni akina nani ? kwa nini wameweka kamera mlangoni kwa Penny.Mle ndani waliingia kufanya nini? Akawaza huku akiendelea kuwatazama wale wale jamaa katika runinga.
“ Hapa kuna jambo ambalo si la kawaida.Watu hawa wamekuja wakiwa na bastora mkononi na tena wanaonekana ni watu makini na wazoefu.Mhh! suala hili si dogo kama ninavyolifikiri.Tayari nimepata sehemu ya pili ya kufanyia uchuguzi .Natakiwa kuwafahamu watu hawa ni akaina nani, na nini lengo la kuja kwa Peniela wakati mwenyewe hayupo.” Akawaza Mathew na kuprint zile picha za wale jamaa.
“Bado sipati jibu watu wale ni akina nani na kwa nini wameweka kamera nyumbani kwa Penny.Nadhani lengo lao ni kufuatilia kila kinachoendela pale. Inaonekana kuna watu ambao wanafuatilia nyendo za Penny na walifahamu fika kwamba kwa muda huu hayupo nyumbani ndiyo maana wakaingia na kufanya walichotaka kukifanya.Watu hawa lazima niwafahamu na nini lengo lao kwa Penny.Ninaanza kuwa na wasi wasi sana kuhusiana na maisha ya Penny.Inaonekana yuko katika hatari kubwa.Kuna watu wanaomfuatilia ambao sijui lengo lao ni nini .Penny yuko wapi? Kwa mujibu wa Jason ni kwamba siku ya pili leo Penny hajulikani yuko wapi .Kesho nitaanzia kazi kwa Penny.Lazima nifahamu yuko wapi ” Akawaza Mathew na kuondolewa katika mawazo na simu iliyoita.Zilikuwa ni namba ngeni katika simu yake
“ Hallow ! akasema
“ Hallow kaka,kuna mtu anahitaji kuongea nawe.” Ikasema sauti ya upande wa pili.Baada ya sekunde kadhaa akasikia sauti tamu ambayo aliitambua mara moja
“ Hallo Mathew” ikasema sauti ile
“ Anitha ! akasema Mathew
“ Niko hapa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere”
“ Ouh gosh ! Kwa nini hukuniambia utaingia muda gani ili nije nikupokee?
“ Hapana sikutaka kukusumbua Mathew.Hapa ni nyumbani.Nisubiri hapo hapo nyumbani nitachukua taksi” akasema Anitha na kukata simu.
“ The hacker is here…” akasema Mathew kwa sauti ndogo huku akitabasamu.
“ Bado Noah.yeye aliniambia anakuja kesho.Kazi imeiva” akawaza Mathew huku akiendelea kuziangalia picha mbali mbali zilizokuwa zinapita katika runinga zilizokuwamo mle ndani.
**********
Penny alijiangalia katika kioo kikubwa ,kugeuka nyuma akajitazama na kutabasamu
“ Siku zote huwa sina wasi wasi na uzuri wangu” akasema Penny kwa sauti ndogo huku akiikoleza rangi ya mdomo.Akachukua kichupa kidogo cha uturi na kudondoshea matone machache shingoni.
“ Leo lazima Dr Joshua atapagawa na mimi.Ni muda mrefu sana hajakutana nami.Nitampa vitu adimu ambavyo vitampagawisha na kumchanganya .Huu ni wakati wa kutumia kila aina ya ujuzi nilionao ili niweze kuimaliza kazi” akawaza Penny huku akichukua mkoba wake mdogo na kufungua mlango.Nje ya mlango wake alisimama kijana mmoja aliyevalia nadhifu.
“ Uko tayari? Akauliza Yule kijana
“ Ndiyo niko tayari.Tunaweza kwenda” akasema penny na kuongozana na Yule kijana mpaka katika gari moja la kifahari akafunguliwa mlango na kuingia kisha wakaondoka.
“ Najua Jason na Jaji Eklibariki watakuwa wamenitafuta sana baada ya kutoniona kwa siku ya pili leo.Natamani niwataarifu kwamba niko salama lakini naogopa kwani Kareem alinionya nisimpigie simu mtu yeyote na kumfahamisha kwamba niko Arusha.” Akawaza Penny akiwa garini
“ Sijui wamefikia wapi ule mpango wao wa kumtafuta muuaji wa Edson.Nikirudi nitawashauri waachane na jambo hili kwani lina mkanganyiko mkubwa na ni hatari kwa usalama wao.Sitaki yeyote kati yao apatwe na tatizo lolote.Hawa ni watu wangu wa muhimu sana bila wao hivi sasa ningekuwa ninakula maharage ya jela. ” Akaendelea kuwaza na mara picha ya Jason ikamjia kichwani .
Saa tatu na dakika arobaini wakawasili Meru view hotel,moja kati ya hoteli kubwa sana afrika mashariki na kati.Ni katika hoteli hii ndipo alipofikia rais wa jamhuri ya mungano wa Tanzania Dr Joshua tayari kabisa kwa ajili ya kuongoza kikao cha wakuu wa nchi za afrika msahariki kinachotarajiwa kufanyika jijini Arusha kwa muda wa siku tatu.Ulinzi ulikuwa mkali sana kuizuguka hoteli hii na kila gari lililoingia hapa ililazimika kukaguliwa na askari.Gari alilopanda Penny halikukaguliwa likapita moja kwa moja hadi katika maegesho ya viongozi wakuu mlango ukafunguliwa na Penny akashuka.
“ Wow ! what a beautiful place” akawaza Penny huku akitabasamu akiifurahia mandhari ile ya kupendeza ya hoteli ile kubwa.Yule kijana ambaye hakuwa muongeaji alimuongoza Penny hadi katika mlango wa nyuma wakaingia ndani ya hoteli na kwa kutumia lifti wakapanda hadi ghorofa ya sita wakashuka na kulifuata varanda refu.Hakukuwa na mtu anayeranda randa katika ghorofa hii zaidi ya walinzi wa rais ambao walikuwa makini na kila aliyeonekana eneo hili. Hakuna kati yao aliyethubutu kumuuliza chochote Penny kwani alikuwa ameongozana na mmoja wa walinzi wa rais.Moja kwa moja akampeleka Penny hadi katika chumba cha rais akagonga mlango ukafunguliwa na Kareem mlinzi wa rais.
“ Penny karibu ndani” akasema Kareem huku akimshika mkono na kumuelekeza aketi sofani.Kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri mno.Kwa muda wa sekunde kadhaa Kareem aliendelea kuchezea simu yake halafu akainua kichwa na kusema
“ Unatumia kinywaji gani Penny?
“ Nipatie mvinyo tafadhali” akasema Penny.Kareem akamletea chupa ya mvinyo na kumuwekea mezani
“ Mheshimiwa rais bado yuko katika kikao.Utaendelea kumsubiri” akasema Kareem na kuendelea kuchezea simu yake kubwa
“ How’ve u been Kareem? Maisha yako yanakwendaje? Akaamua kuanzisha maongezi Penny baada ya kuona Kareem amekuwa kimya sana na ilionyesha hakutaka maongezi
“ I’m ok Penny.I’m doing fine.Samahani kama umeboreka lakini niko kazini.Tuna marais karibu watano watahudhuria mkutano mkubwa wa marais wa afrika mashariki kuanzia kesho kwa hiyo yatubidi tuwe macho sana katika ulinzi ndiyo maana unaniona nimekuwa kimya sana nafuatili akila kinachoendelea hapa hotelini”
“ Usijali Kareem.Ninaelewa” akasema Penny na kuelekeza macho yake runingani akitazama muziki
“ Kareem ! akaita Penny baada ya muda
“ Unasemaje Penny? Akauliza Kareem
“ Nitakuwepo hapa Arusha kwa muda gani?
“ As long as present wants” akajibu Kareem, kwa ufupi
“ No Kareem.I need to go back to Dar as soon as possible.” Akasema Penny
Kareem hakumsemesha kitu akaendelea na kazi zake
Saa sita na dakina nane mlango wa chumba cha rais ukafunguliwa na Dr Joshua rais wa jamhuri ya muungano akaingia
“ Where is she? Akamuuliza Kareem ambaye alimfanyia ishara kwamba tayari yuko chumbani
“ Thank you Kareem.Thank you so much.From now I need a privacy.No calls no any disturbance” akasema Dr Joshua
“ Ok Mr President” akajibu Kareem kwa adabu.Dr Joshua akakinyonga kitasa cha mlango na kuingia chumbani kwake.Ilimlazimu avue miwani yake ili ajiridhishe kwamba alichokuwa akikiona kitandani binadamu wa kawaida na si malaika .Kiumbe kilichokuwa kimejilaza katika kitanda kilichotandikwa mashuka mazuri meupe kilikuwa na uzuri usio wa kawaida.
“ Penny ! akaita
“ Dr Joshua ! akasema Penny kwa sauti ndogo.Dr Joshua akafunga mlango na kumuendea Penny akamkumbatia kwa nguvu
“ Welcome back my angel” akasema Dr Joshua .Penny hakutaka kupoteza muda akammwagia mzee Yule mabusu mfululizo na kumchanganya. Dr Joshua akajikuta akianza kuhema kwa nguvu.Taratibu akatoa ulimi na kuuingiza kinywani kwa Dr Joshua ambaye alianza kutoa miguno.Penny akamvua koti taratibu huku akiendelea kumfanyia manjonjo yaliyozidi kumpagawisha Dr Joshua. Taratibu akalegeza tai na kuitoa halafu akaanza kufungua vifungo vya shati .Alikichezea kifua cha mzee yule kwa ufundi mkubwa halafu akaufungua mkanda wa suruali yake ikaanguka chini akabakiwa na nguo ya ndani,Penny akaivuta taratibu nguo ile ya ndani akaishusha hadi magotini halafu akapiga magoti na kuanza kufanya utundu maeneo ya ikulu.Dr Joshua hakuwa akijiweza tena.Penny akamsukuma akangukia kitandani halafu akafungua zipu ya gauni lake likaanguka chini.Dr Joshua mate yakamtoka alipoushuhudia mwili mwororo wa kimalaika wa msichana aliyesimama mbele yake.Taratibu akaivua nguo yake ya ndani na kupanda kitandani na kuendeleza utundu.Dr Joshua alibaki akilalama kwa raha alizokuwa akipewa.Baada ya dakika kumi na tano tayari walikuwa wakiogelea katika ulimwengu wenye raha isiyoelezeka.
*******
“ Ouh Peniela..nakosa neno la kusema kwa raha ulizonipa.I missed you .I missed this….” Akasema Dr Joshua akiwa hoi baada ya kumaliza mzunguko mmoja.Penny akajiinua na kumsogelea akambusu na kukilaza kichwa chake kifuani
“ I missed you too Dr Joshua..Umri umekwenda lakini bado una nguvu kama kijana wa miaka kumi na nane.You make me so happy” akasema Penny
“ Muda wote uliokaa gerezani ukikabiliwa na kesi nilikosa raha na amani.Kwa sasa najiona kijana tena.You are amazing my angel” akasema Dr Joshua huku akizichezea nywele za Penny
“ Don’t lie to me Dr Joshua.Kama ningekuwa na umuhimu kwako usingekubali kuniona nikiteseka gerezani mwaka mzima kwa kosa ambalo sikulitenda na zaidi ya yote ulishinikiza nifungwe kifungo kirefu gerezani.You didn’t stand by my side.Pamoja na mateso yote na hata kunusurika kwenda maisha gerezani lakini sikufumbua mdomo wangu na kuongea lolote kuhusiana na kifo cha Edson.Ninajua wewe ndiye uliyeamuru watu wako wamuue Edson kwa sababu unazozijua mwenyewe lakini kwa kuwa ninakupenda Dr Joshua mpaka leo hii hakuna mtu anayefahamu chochote” akasema Penny na machozi yakamtoka alipomkumbuka Edson.Dr Joshua akamfuta machozi na kusema
“ Tafadhali usilie Penny.Usilie malaika wangu.Kuna mambo mengi ambayo yametokea kitu cha kwanza ninachokihitaji toka kwako ni msamaha wako.Ni kweli nilikuacha ukaingia katika matatizo makubwa na sikusimama pamoja nawe.Penny please forgive me my angel.We have so many to talk” akasema Dr Joshua.Penny akainua kichwa akamtazama na kusema
“ Nimekwisha kusamehe Dr Joshua na ndiyo maana niko hapa.Umesema tuna mambo mengi ya kuongea hata mimi nina mengi ya kuuliza lakini kwanza nataka unieleze kwa nini Edson aliuawa? Akauliza Penny.Dr Joshua akachukua kitambaa na kujifuta jasho,akainuka na kwenda mezani akajimiminia mvinyo na kupiga funda kubwa.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………
No comments
Post a Comment