PENIELA (Season 1 Ep 21)
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Dr Flora hakutikisa hata ukope.Haraka haraka Winifrida akakimbilia katika simu akampigia Captain Amos daktari wa familia ya rais ambaye alifika mara moja na vipimo akampima na kuamuru liitwe gari la wagonjwa haraka.Gari la wagonjwa likafika Dr Flora akapakiwa na kukimbizwa katika hospitali ya jeshi.Pale akapimwa na kukutwa tayari amekwisha fariki.Baada ya kuthibitishwa kwamba amefariki dunia Captain Amos akampigia simu Dr Joshua
“ Hallow Captain” akasema Dr Joshua
“ Mr President its done.She’s dead”
“ Thank you Captain Amos.Niko njiani narejea Dar es salaam” akasema Dr Joshua na kukata simu.Captain Amos alibaki amesimama ameegemea mti.Alikuwa na mawazo mengi sana.
“ I’ve killed the first lady…Please forgive me lord” akawaza Captain Amos
ENDELEA…………………………
Ndege aliyopanda Peniela akitokea jijini Arusha ilitua katika uwanja wa ndege wa kiataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam .Pale uwanjani kulikuwa na gari mbili zimeandaliwa kwa ajili yake .Moja ikiwa ni kwa ajili ya yeye kupanda na nyingine ilikuwa na walinzi wanne wa kumlinda.Baada ya kuingia katika gari akaomba apelekwe moja kwa moja katika nyumba ambayo Dr Joshua alimtaka ahamie mara tu atakaporejea Dar es salaam.
“ Nimerejea Dar es salama kama malkia.Naya penda maisha haya lakini ni kwa muda mfupi tu.” Akawaza penny akiwa garini.Uso wake haukukaukiwa na tabasamu .
Waliwasili katika jumba ambalo Dr Joshua alikuwa amempatia.Lilikuwa ni jumba kubwa zuri la kifahari la ghorofa tatu lililokuwa kandoni mwa bahari ya Hindi.Toka lilipojengwa halikuwahi kukaliwa na mtu yeyote.Alifunguliwa mlango na kuingia ndani,ambako kulikuwa na uzuri wa kipekee.Kulikuwa na samani za kupendeza za hali ya juu za gharama kubwa bila kusahau nakshi mbali mbali za kuvutia mno.Alishindwa kuizuia furaha yake pale alipoingia katika chumba cha kulala.
“ Wow ! This is amazing” akasema kwa furaha.Kilikuwa n i chumba kikubwa na kizuri mno chenye kila kitu cha thamani ambacho angehitaji kiwepo chumbani.Alienda katika dirisha kubwa na kuishuhudia madhari ya kupendeza ya bahari ya Hindi
“ This place is like paradise” akasema
“ Nimeipenda sana hii nyumba ni nzuri mno.Ina kila kitu ninachokihitaji” akasema Penny huku ajkishuka na kwenda kuangalia muonekano wa n je.Nje ya jumba lile la kifahari kulikuwa na viwanja vya michezo mbali mbalikama kikapu ,tenisi na wavu.Kulikuwa pia bwawa la kuogelea na bustani nzuri yenye maua na miti ya kupendeza.Lilikuwa ni jumba la kifahari mno.
“ Nimelipenda mno jumba hili na ninatamani kama ningeishi hapa lakini sintoweza.Nlimkubalia Dr Joshua kule Arusha lakini ni vigumu sana kwa mimi kukaa hapa.Sina mpango wa kuwa na mahusiano ya muda mrefu na yeye.Baada tu ya kazi yangu kumalizika mimi na yeye hatutakuwa na mahusiano tena.Uhusiano wetu utakuwa umefikia mwisho.” Akawaza Penny akiwa njiani kueleka nyumbani kwake
“ Natamani nifahamu jaji Elibariki na Jason wamefikia wapi kuhusiana na mpango wao wa kufanya uchunguzi juu ya kifo cha Edson.Sitaki waendelee na mpango wao ule kwa sababu ni hatari kubwa kwao.Sitaki wapate madhara yoyote yale kwani ni watu wangu wa karibu na wana umuhimu mkubwa katika maisha yangu. Kwa maana hiyo basi itanilazimu kutafuta namna nitakayoweza kuwafanya wasiendelee na mpango wao ule.Lazima niuvuruge ili kuwasaidia “ akawaza
Aliwasili nyumbani kwake akafunguliwa geti na kuingia ndani .Akaagana na wale walinzi wakaondoka.
“ Home sweet home”akasema kwa furaha alipoingia tena katika sebule yake
“Ninaipenda mno nyumba yangu na katu siko tayari kwenda kuishi sehemu nyingine”akawaza huku akipiga hatua kuelekea chumbani kwake.
Mara tu alipoingia chumbani kwake alipatwa na mstuko wa ghafla.Aligundua vitu havikuwa sawa.
“ Someone was here.Kuna mtu aliingia humu ndani ” akasema kwa hasira na woga
“ Vitu vyangu haviko sawa kama nilivyoviacha.Kuna mtu alikuja kupekua nyumba yangu.Atakuwa nani huyu ? Kitu gani walikuwa wanatafuta? Akawaza Penny akiwa amekasirika kupita kiasi na mara akakumbuka kitu,akaiwasha kompyuta yake na kupitia anuani yake ya barua pepe akaziona picha za mtu aliyefungua kasiki lililokuwa ukutani.Kasiki lle lilikuwa na kamera ya siri ambayo huchkua picha ya kila anayelifungua na kuirusha moja kwa moja katika anuani ya parua pepe ya Peniela.
“ Bastard !! akasema Penny kwa hasira baada ya kuiona picha ya jamaa mmoja aliyevaa glovu nyeusi mikononi akiwa ameshika heleni zake alizokuwa amezihifadhi katika kasiki
“ It’s them !!..”akasema na kuvuta pumzi ndefu
“ Kitu gani awlikuwa wakikitafuta humu ndani?.Watu hawa sasa wameanza kunichosha.Nilipatwa na matatizo na kunusurika kuingia gerezani lakini hawakunisaidia lolote.They are monsters.” Akawaza na kukaa kitandani
“Najilaumu sana kuingia katika kazi hii.Kwa sasa siwezi tena kujiengua.They have me in their hands.They control me” akainama na kudondosha chozi
“ kama ingekuwa ni kwa ridhaa yangu basi nisingekubali kujiunga nao .Nimekasirishwa mno na kitendo chao cha kuingia ndani mwangu na kupekua bila ruhusa yangu.Huu ni ukosefu wa adabu na ustaarabu.Ninafanya kazi zao vizuri lakini bado hawataki kuniacha walau niwe na maisha ya kawaida.Nilitegemea baada ya kumaliza mwaka mzima nikiwa gerezani nikiendelea na kesi yangu wasingesumbuka nami tena lakini walipofahamu nimeshinda kesi mara moja wakaendelea kuniandama na kunitaka niendelee na kazi yao .I’m tired with this life.I’m tired with them.Baada ya kazi hii kumalizika sitaki tena kufanya kazi yoyote tena.Chochote kitakachotokea na kitokee tu lakini nimechoka sasa.I need to live a normal life.I need my freedom back.” Akawaza Penny na mara akastuliwa na mlio wa simu ya mezani.Katika meza ya simu kulikuwa na simu tatu na iliyokuwa ikiita ilikuwa ni simu ya rangi nyeusi.
“ Its them ! akasema kwa hasira nakuichukua simu ile akabonyeza kitufe cha kupokelea
“ hallow “ akasema kwa sauti ya juu yenye kuonyesha wazi alikuwa amekasirika
‘ hallow Peniela” Ikasema sauti ya upande wa pili.Penny akastuka kidogo kwani haikuwa ile sauti aliyoizoea
“ Welcome back Peniela” akasema tena Yule jamaa upande wa pili
“ Who are you ? and where is he? Akauliza Penny
“ Relax penny.From now on you’ll be talking to me.My Code is 00P688.Muda wowote ukiwa na shida yoyote kubwa na unahitaji ufumbuzi au msaada wa haraka nitafute kwa kutumia code hiyo na utasaidiwa haraka sana.By the way where were you? Akauliza Yule jamaa ambaye alikuwa akiongea kwa taratibu sana
“ Kwa nini nyumba yangu imepekuliwa ? Don’t you trust me? Akauliza Penny kwa ukali
“ I’m sorry penny ,lakini ulipotea ghafla na hatukujua uko wapi kwa hiyo ni jukumu letu kuhakikisha kwamba uko salama na ndiyo maana tukaingia ili kufahamu kama umepatwa na tatizo lolote.Ni jukumu letu kuhakiki usalama wako Penny”
“ Naomba iwe ni mwanzo na mwisho kuingia ndani mwangu wakati sipo na wala sitaki kufuatiliwa na mtu yeyote Yule.Ninafanya kazi zangu vizuri kama mnavyotaka kwa hiyo naomba msivue mipaka.” Akasema Penny kwa ukali
“ Ok nimekuelewa Penny lakini siku nyingine kama una safari au unahitaji faragha, nitaarifu nifahamu li tujue kwamba uko salama.Vipi kuhusu mahusiano yako na mheshimwa rais yakoje toka umemaliza kesi?Mmeonana tayari? Akauliza Yule jamaa ambaye hakutaka kujitambulisha jina
“ Mahusiano ni mazuri,tunaendelea vizuri.Tayari nimekwisha mrudisha katika mstari na sasa ninaweza kuendelea kuimalizia kazi yangu.”
“ Ok vizuri penny.Jitahidi kwenda kwa kasi kidogo kwa sababu muda uliopangwa kwa operesheni hii unakaribia kumalizika na tusipofanya haraka kilakitu kitavurugika.” Akasema Yule jamaa
“ Hii si kazi rahisi kama mnavyodhani na haiwezi kwenda kwa haraka kama mnavyotaka.Inahitaji kutumia akili sana ili kuikamilisha kwa hiyo naombeni msiniharakishe.Niacheni niifanye kazi hii kadiri ninavyoona inawezekana.Pale ikulu si kama uwanja wa disko.Ile ni sehemu ngumu mno kuingilika kwa hiyo kuweni na subira” akasema penny
“ Nakuelewa penny lakini operesheni hii imechukua muda mrefu sana tofauti na tulivyokuwa tumeipanga.Na hii ilisababishwa na wewe kusahau kazi yako na kujiingiza katika masuala ya kimahusiano hadi kupelekea ukakutwa na yale matatizo.Jitahidi operesheni hii i malizike haraka kwani bado kuna kazi nyingi zinakusubiri” akasema Yule jamaa na kumstua Penny
“bado kuna kazi nyingine? I’m sorry guyz,nikisha kamilisha kazi hii nahitaji mapumziko.I need a break .I need back my normal life” akasema penny
“ Hahahaa..!! Penny we don’t have normal life and we don’t have time to rest.We workd day and night to make sure the nation is safe and people live their normal life.That means we’ve sacrificed our life for the people of this nation.Without us they cant sleep,so forget about break !.Nahitaji kuuona mpango kazi wako kabla ya saa mbili usiku leo ili nione kama unaenda katika njia sahihi.” Akasema Yule jamaa
“ Ok nitakutumia mpango kazi lakini ni baada ya siku mbili.Kuna mambo ambayo lazima niyaweke sawa kwanza.” Akasema penny
“ hakuna siku mbili Peny.Nahitaji leo kablaya saa mbili usiku uwe umenitumia.! Akasema kwa sauti ya juu Yule jamaa
“ tafadhali naomba usiniamrishe namna hiyo.You don’t know what I’m going through right now.You all depend on me to complete this mission so you’ll have to listen to me.Nimesema nitakutumia baada ya siku mbili and that’s final” akasema Penny
“ Ok Peny ,One more thing ,usiache kuvaa heleni yako hata siku moja.Ile ndiyo njia peke e ya mawasiliano kati yetu na wewe.” Akasema Yule jamaa na kukata simu.Penny alikuwa akitweta kwa hasira.Yule jamaa alikuwa amemchefua sana.
“ Who is this guy? Yule wa zamani amekwenda wapi? Akajiuliza.
“ Sifahamu nimepata wapi ujasiri wa kubishana na mtu huyu.These people controls me all over.when will I be free? When I will live a normal life? ..akawaza Penny
Akiwa amejilaza kitandani mwingi wa mawazo simu anayoitumia kuwasiliana na rais ikaita
“ Huyu mzee atapata uchizi mwaka huu.Kila wakati anataka kuongea na mimi” akawaza Penny halafu akabonyeza kitufe cha kupokelea
“” Hallow Dr Joshua”akasema
“ Hallo Penny.Umeshafika?
“ Ndiyo nimekwisha fika Dr Joshua na kwa sasa niko kitandani nimepumzika”
“ Ok pole na safari.Ulikwenda kuiona nyumba?
“ Ndiyo,nilikwenda kuiona.Ni nyumba nzuri mno.”
“Umeionaje inakufaa? kama haikufai niambie nikupatie nyingine.Ninazo nyumba nyingi tu hapa jijini”
‘ Dr Joshua nyumba ile ni nzuri mno na ni nyumba ya ndoto zangu.Ina kila kitu ninachokihitaji na kukipena katika nyumba”
“ nafurahi kusikia hivyo Penny.Nifahamishe una hamia lini?”
“ Dr Joshua I’m sorry.Sintoweza kuhamia katika ile nyumba”
“ kwa nini penny? Mbona tulikwisha kubaliana uhamie pale ili iwe rahisi kwa mimi kufika muda wowote ninaoutaka?
“ Nimebadili mawazo Dr Joshua.Baada ya kuiona nyumba ile nimegundua kwamba siwezi kuishi pale.Its too big for me. I need normal and simple house” akasema Penny
“ Penny my angel wewe ni mwanamke ninayekupenda kuliko ninavyoweza kukueleza.Nina mipango mikubwa sana juu yako.Nataja uishi maisha kama ya malikia.I am the president of United republic of Tanzania and I can give you anything you want.Nataka upate kila starehe ya dunia hii.Tafadhali naomba ukubali kuuishi katika ile nyumba Penny” akasema Dr Joshua
“ Dr Joshua nadhani unafahamu toka tumefahamiana sijawahi kukutamkia neno hapana.Nimekuwa mtu wa kusema ndiyo kwa kila jambo unaloniambia lakini leo naomba niseme hapana.Sintoweza kuishi katika ile nyumba.Nitaendelea kuishi hapa katika nyumba yangu hii ndogo”
“ Ok Penny kama unapenda kuendelea kuishi hapo niruhusu basi niifanyie ukarabati mkubwa ili iwe na mandhari ya mke wa rais.Please don’t say No Peniela”
Peniela akatabasamu na kusema
“ Siwezi sema ndiyo kwa haraka Dr Joshua .Let me think about it” akasema penny
“ Ok Ahsante Penny.Halafu kuna jambo nataka nikutaarifu”
“ jambo gani Dr Joshua?
“ My wife is dead”
Kimya cha sekunde kadhaa kikapita,Penny akauliza
“ When did this happen?
“ Amefariki mchana huu.Hivi sasa niko katika maanadalizi ya kurejea Dar es salaam.”
“ So sorry for your loss Dr Joshua.”
“ Thank you so much the next first lady.Nitakupigia simu baadae .I have to go ,ndege iko tayari”akasema Dr Joshua na kukata simu.
“ Dr Flora is dead ?! This is weird! Amekufa kwa ugonjwa gani? Nilimuona siku ya hukumu ya kesi yangu alikuwa mzima wa afya akiwa ameongozana na wanae,iweje afariki ghafla namna hii? Akajiuliza penny
“ Lakini mbona Dr Joshua haonyesi kuguswa na kifo cha mkewe? Anaongea nami kama vile hakuna kilichotokea na hapo hapo anafanya utani kwa kuniita the next first lady.Si mara moja amekuwa akinitamkia kauli hii ya kwamba mimi ni mke wa rais mtarajiwa.Alijua kwamba mkewe atafariki muda si mrefu ? .Ninapatwa na mashaka kuhusianana kifo hiki cha Dr Flora”akawaza Penny halafu akachukua simu na kumpigia simu Jason akamfahamisha kwamba tayari amekwisha rejea.
*******************
Jaji Elibariki alikuwa akijiandaa kutoka ofisini kwake ili akakutane na akina Mathew waliokuwa wamemtaka aonanenao kuhusiana na ile fedha wanayoihitaji, mara simu ikaita.Akaitazama na kukuta ni mkewe Flaviana ndiye alipiga
“ Flaviana leo kaamua kunipigia simu !..Kashangaa
“ Yawezekana hasira zake zimekwisha ? Akajiuliza
“ kwa dharau alizonionyeshea sina hamu naye tena.”akawaza jaji Elibariki huku akivaa koti lake na kuiacha simu ikiita na kukatika bila kuipokea..Ikaanza kuita tena na kumlazimu aipokee
“hallow” akasema
“ hallow” ikasikika sauti ya Flaviana lakini ilionyesha kana kwamba analia
“ Flaviana why are you calling? akauliza jaji Elibariki huku sura yake ikiwa imekunja ndita kuonyesha kwamba hakupendezwa na simu ile ya mkewe.Flaviana hakujibu kitu akaendelea kulia
“ Flaviana kinachokuliza kitu gani? Kama huwezi kunieleza kilichokufanya ukanipigia simu I’m going to hang up now.I have so many things to do” akasema Jaji Elibariki
“ My mother is dead” akasema Flaviana
“ What ?!!!..jaji Elibariki akastuka
“ My mother…Is dead”akasema tena Flaviana
Jaji Elibariki akapatwa na mstuko mkubwa. Kwa sekunde kadhaa akabaki kimya halafu akauliza
“ Amefariki saa ngapi?
“ Mchana huu”
“ Uko wapi sasa hivi? Akauliza Jaji Elibariki
“ kwa sasa niko hapa katika hospitali kuu ya jeshi” akasema Flaviana
“ Ok ninakuja hapo sasa hivi” akasema jaji Elibariki huku akifuta kijasho kilichoanza kumchuruzika.Taarifa ile ya kifo cha Dr Flora ilimstua sana.
“ Nini kimemuua Dr Flora ghafla namna hii? Nafahamu alikuwa akisumbuliwa na shinikizo la damu lakini hali yake haikuwa mbaya na jana usiku nilimsikia akizungumza na mwanae.” Jaji Elibariki alikuwa amekaa mezani akiwaza .Akachukua simu na kumpigia simu Jason akampa habari zile na kumtaka aende akaonane na akina Mathew ili alijadili suala lile la pesa wanazozihitaji,yeye akapanda gari na kuelekea hospitali kuu ya jeshi .
Aliwasili katika hospitali kuu ya jeshi na kukuta magari mengi yameegeshwa.Ulinzi ulikuwa mkali sana na watu haakuruhusiwa kuingia ndani bila sababu maalum.Alijitambulisha getini kama jaji wa Mahakama kuu na mume wa Flaviana mtoto wa Rais,akaruhusiwa kupita.Aliegesha gari na akashuka na kuangaza huku na huku akijaribu kumtafuta mkewe mara akamuona Genevive binamu yao akina Flaviana.Wakasalimiana na kumuuliza mahala aliko Flaviana.
“ Sina hakika kama unaweza kuonana naye muda huu.Amepumzishwa katika chumba alikuwa amepoteza fahamu baada ya kuonyeshwa mwili wa mama yake”
“ Nipeleke mahaal alipo.I need to see her” akasema Jaji Elibariki.Genevive akamuongoza hadi katika chumba ambacho Flaviana alikuwa amepumzishwa.Nje ya mlangow a chumba kile alikuwepo muuguzi aliyekuwa akizuia mtu yeyote asiingie mle chumbani kama si daktari.Jaji Elibariki akajitambulisha kama mume wa Flaviana na kuruhusiwa kupita.Flaviana alikuwa amelala kitandani na alipomuona mumewe akaangua kilio.Jaji Elibariki akamfuata pale kitandani akamkumbatia na kumfariji
“ Pole sana Flaviana.” Akasema.
“ Eli,mama yangu amekwenda.” Akasema Flaviana huku akilia
“ Tafadhali usilie Flaviana.Its gonna be ok.I’m right here” akasema jaji Elibariki huku akimfuta mke wake machozi .
“ Nini kimesababisha kifo cha mama? Akauliza jaji Elibariki
“ Mpaka sasa hivi hatufahamu chochote kuhusiana na nini kimemuua.Madkatari bado hawajasema chochote lakini daktari wa familia Captain Amos anasema ni shinikizo la damu.Eli,inaniuma sana kumpoteza mama yangu.Jana usiku nimeongea naye akanipigia simu na kuniambia kwamba leo anahitaji kuonana nasi mimi na Anna kuna jambo la maana mno anataka kutueleza lakini kabla ya kuonana naye amefariki dunia ghafla.Inauma sana Eli.Ninaumia mno”
“ Pole sana Flaviana” akasema Jaji Elibariki na kuendelea kumbembeleza mkewe.
“ Jambo gani alilotaka kuwaambia?
“ Sifahamu Eli,sijui alitaka kutuambia nini lakini alisisitiza mno.Inaonekana alikuwa na jambo kubwa la kutueleza.” Akasema Flaviana na kuendelea kulia
“ Kifo cha ghafla cha Dr Flora hata mimi kinanipa mashaka mno.Alitaka kuwaeleza nini wanae? Kwa nini afariki ghafla kabla hajakutana na wanae? Kuna maswali mengi sana ya kujiuliza kuhusiana na kifo hiki” akawaza Jaji Elibariki
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
TUNAWATAKIA NYOTE WEEKEND NJEMA…
No comments
Post a Comment